Home » » SERIKALI ya Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi imewaagiza maofisa ugani kuwaelimisha wananchi ili waweze kufanya mageuzi mageuzi ya kilimo chenye tija

SERIKALI ya Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa Katavi imewaagiza maofisa ugani kuwaelimisha wananchi ili waweze kufanya mageuzi mageuzi ya kilimo chenye tija

 
Na  Walter   Mguluchuma .
  Katavi



SERIKALI  ya  Wilaya  ya   Tanganyika   Mkoa  wa   Katavi imewaagiza
maofisa ugani  kuwaelimisha  wananchi  ili  waweze kufanya  mageuzi
mageuzi ya kilimo chenye tija   kwa kulima mazaomengine ya biashara
badala  ya kutegemea zao moja tu  la tumbaku .

Agizo hilo lilitolewa na Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika  mkoani Katavi ,
Salehe Mhando  wakti alipokuwa  akizungumza   na watumishi  wa wilaya
yake  , akisisitiza kuwa  wakati  sasa umewadia kwa wakulima wilayani
humo  kuanza  kulima  mazao  ya kahawa  na ufuta kama mazao  ya
biashara  badala  ya kutegemea zao  moja la tumbaku .

“Wakulima wetu  wanalima  zao  la tumbaku  kama zao  la biashara  pia
mahindi  kwa ajili  ya chakula  na kama zao  la biashara ….. hali ya
hewa  ya wilaya hii  haitofautiani  na  ile  ya  mikoa  inayostawisha
ufuta  na kahawa kwa wingi

….. hivyo  ni vema  maofisa ugani  wetu wakaanza kuwahamasisha  kulima
 ufuta na kahawa ili kupanua wigo  wa mazao  ya  biashara  ambayo
yaataongeza kipato kwa mkulima mmoja mmoja  na taifa kwa  ujumla wake
“ alisisitiza.

Aliwaeleza watumishi hao  kuwa Serikali  ya Wilaya  ya Tanganyika
imejipanga kutekeleza   ahadi  za   miradi ya   maendeleo  zilizomo
katika   Ilani  ya   Uchaguzi   zilizohaidiwa   wakati wa   Kampeni za
 Uchaguzi Mkuu  uliopita   na   zilizotolewa  ambazo   haziko  kwenye
 Irani  hiyo ..

 Alisema  jamii   imebadilika  inataka   kushuhudia  vitendo na sio
porojo  akiwatak  maofisa mipango wafanye   kazi kwa  vitendo   ili
kuhakikisha  kuwa  wilaya hiyo  inakuwa na vipao mbele vyake .

Alizianisha changamoto  zinazoikabili wilaya  hiyo ikiwa ni pamoja na
uhaba wa maji safi na salama , upungufu wa vituo  vya afya  vilivyopo
ni vitatu  huku kata zikiwa 16  pia uhaba  wa vyumba vya madarasa kwa
shule za msingi   ambapo wanafunzi wanalazimika  kusomea nje  huku
akisisitiza kuwa  lazima  kila  shule ihakikishe inajenga  vyumba vya
madarasa vinne  hadi  ifikapo Desemba mwaka  huu ..

Alisema   kwa  upande  wa  shule  za   Sekondari  zipo kata   sita
ambzo   hazina   shule   za   Sekondari   huku   mpango wa  serikali
ukisisitiza  kila  Kata   ijenge     shule   moja   ya    sekondari .

Aidha  ameziagiza Idara  za   ushirika   naIdara  ya   Maendeleo ya
Jamii  kufanya  kazi kwa  kushirikiana kwa   kuwahamasisha   vijana
kuunda   vikundi  ili  waweze  kupatiwa  mkopo   wa  asilimia  tano
zinazotolewa   na  halmashauri   hiyo .

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa