Na Walter Mguluchuma .
Katavi .
Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi imemuhukumu Ally Rashid maarufu Ally Mwizi kifungo cha miaka 30 baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti i kwa nguvu makaburini juu ya kabur i msichana 25 jina limehifadhiwa Mkazi wa Mtaa wa Kotazi Mjini.
Hukumu hiyo iliyovutiwa hisia za watu wengi wa Manispaa ya Mpanda ilitolewa hapo jana na Hakimu Mkazi mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa baada ya Mahakama kulidhika na ushahidi uliotolewa Mahakamani hapo na upande wa mashitaka ulikuwa ukiongozwa na Mwanasheria wa Serikali wa Mkoa wa Katavi Jamila Mziray .
Awali katika kesi hiyo mwandesha mashitaka mwanasheria wa Serikali wa Mkoa wa Katavi Jamila Mziray alidai mahakamani hapo kuwa mshitakiwa Ally Mwizi alitenda kosa hilo hapo hapo june 17 mwaka huu majira ya saa mbili usiku huko katika Makaburi ya Kashaulili yalioko katika mtaa wa Kotazi Mjini hapa .
Ilidaiwa kuwa mshitakiwa kabla ya kutenda kosa hilo alimfuata msichana huyo ambae alikuwa ameibiwa vitu vyake vya ndani ya nyumba hivyo alimdanganya kuwa yeye Ally Mwizi anaouwezo wa kumsaidia kuvipata vitu vyake vilivyoibiwa .
Mziray aliiambia Mahakama kuwa baada ya msichana huyo kuahidiwa na mshitakiwa kuwa vitu vyake alivyoibiwa vitapatikana aliambiwa amlipe ujira Ally Mwizi kiasi cha Tsh 30.000 ili aende akamwonyeshe vitu vyake alivyoibiwa na alifanya hivyo.
Ndipo siku hiyo ya tukio mshitakiwa alimpigia simu msichana huyo majira ya saa mbili ili aweze kumpeleka kwenda kumwonyesha vitu hivyo alivyoibiwa .
Mziray alieleza baada ya kuwa amempigia simu mshitakiwa alikwenda nyumbani kwa msichana huyo na kumchukua na kisha alikwenda nae kwenye makaburi ya Kashaulili kwa lengo la kwenda kumwonyesha vitu alivyoibiwa lakini baada ya kufika makaburini mshitakiwa alipiga ngwala msichana huyo na kisha alianza kumlawiti juu ya kaburi huku akimtishia kumuuwa endapo angepiga kelele .
Baada ya kumaliza haja yake mshitakiwa alimwomba dada huyo waende kwenye nyumba ya kulala wageni inayoitwa Kingi Parisi ili wakaendelee kufanya mapenzi zaidi ya kwa kile alichodai kuwa eneo la Kingi Parisi panafaa zaidi kufanyia tendo la ndoa kuliko juu ya kaburi.
Aliiambia Mahakama ndipo msichana huyo alipoamua kupiga mayowe ya kuomba msaada na watu walifika kwenye eneo hilo na waliweza kumkamata mshitakiwa .
Hakimu MKazi Chiganga Ntengwa akisoma hukumu hiyo aliambia mahakama kuwa kutokana na ushahidi uliotolewa Mahakama hapo pasipo shaka yoyote mahakama imemwona Mshitakiwa Ally Mwizi kuwa amepatikana na hatia ya kifungu cha sheria Namba 154 kidogo cha kwanza ya makosa ya adhabu sura na 16.
Hivyo kutokana na kupatikana na kosa hilo Mahakama imemuhukumu Ally Mwizi kutumikia kifungo cha miaka 30 jela ili akitoka gerezani awe na tabia njema kwenye jamii ya watu .
0 comments:
Post a Comment