Home » » ARFI UKOMO WA UANACHAMA WANGU CHADEMA KUISHA BAADA YA BUNGE KUVUNJWA

ARFI UKOMO WA UANACHAMA WANGU CHADEMA KUISHA BAADA YA BUNGE KUVUNJWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
 Makamu  Mwenyekiti  wa  Taifa  Chama cha  CHADEMA  Tanzania   Bara     alitejiuzuru  Mbunge wa Jimbo la Mpanda Mjini  Said  Amour  Arfi   amewaambia wananchi wa Mji wa Mpanda kuwa uanachama wake  katika   chama cha CHADEMA  utaishia mara   tuu baada ya kuvunjwa Bunge la Jamuhuri ya Muungano  hapo Julai 9  mwaka huu
 Arfi  alitowa kauli  hiyo  hapo  jana wakati  alipokuwa  akiwahutubia  wananchi wa  Mji wa Mpanda  katika  mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye  shule ya msingi Kashato mjini  hapa
Pia  alitumia  mkutano  huu   kuwaaga Wanachi wa Jimbo la Mpanda Mjini  kuwatangazia kuwa hatagombea tena  jimbo  hilo   ambalo  ameliongoza kwa kipindi cha miaka kumi
    Aliwaeleza wananchi hao kuwa  yeye  Arfi   anatarajia  mara ya Rais  Jakaya  Kikwete  kulivunja  Bunge la  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  ndio utakuwa  mwisho wake  kuwa  mwanachama wa  CHADEMA kuanzia  siku hiyo
Alisema  mbalali  ya kujiondoa uanachama  wake  CHADEMA  alitangaza kutogombea ubunge wa Jimbo la Mpanda Mjini ambalo  amekuwa  akiliongoza  kwa vipindi  viwili   kuanzia  mwaka  2005 hadi  sasa
  Arfi alifafanua kuwa  yeye  hayuko tayari kugogombea jimbo hilo kupitia chama  chochote kile cha siasa na kauli hiyo ilemenga kuondoa uvumi uliokuwa umeenea wa kuwa alikuwa na nia ya kugombea kupia ACT au  CCM
 Alisema  amekuwa akishangazwa na kauli  ambazo  zimekuwa zikitolewa na  baadhi ya  wanachana na wapenzi wa CHADEMA kuwa   yeye  hajafanya lolote kwenye  chama  hicho
Kama kuna mtu  anae  kifahamu  vizuri  chama  hicho  basi ni yeye  hivyo  haoni  sababu ya yeye watu kumbeza alikuwa  ameamua kukaa kumya hivyo  akiamua   atamwaga  mboga  iliwatu wafahamu  mapungufu yalioko  ndani ya  chama hicho 
 Alisema  yeye  hagombei  jimbo  hilo na  kama  kweli  chama  hicho  kinanguvu  basi  watetei  jimbo hilo  ambalo alikuwa analiongoza yeye ila  nao  uhakika    jimbo  hilo  litakwenda  CCM kwani  wananchi wa jimbo  la  mpanda mjini  walikuwa na mapenzi na mtu sio  chama

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa