TAKUKURU KATAVI WAPOKEA JUMLA YA MALALAMIKO 78 YA VITENDO VYA RUSHWA NA MAJALADA 115 YANACHUNGUZWA.

WAZIRI MKUU MSTAAFU MIZENGO PINDA ASHUHUDIA MAKABIDHIANO YA MWENGE MKOANI KATAVI

 WAZIRI MKUU MSTAAFU MIZENGO  PINDA AKISALIMIANA NA MKUU WA MKOA WA TABORA AGREY  MWANRI KWENYE UWANJA WA NDEGE WA MPANDA  WAKATI WA MAKABIZIANO YA MWENGE WA UHURU YALIOFANYIKA  JANA KATIKA UWANJA WA NDEGE WA MPANDA KUFUTIA MWENGE WA UHURU KUMALIZA MBIO ZAKE KATIKA MKOA WA TABORA NA KUKABIDHIWA KWA VIONGOZI WA MKOA WA KATAVI BAADA YA KUSAFIRISHWA KWA NDEGE KUFUATIA BARABARA INAYOIUNGANISHA MIKOA HIYO KUFUNGWA KUTOKANA NA DARAJA LA MTO KOGA KUJAA MAJI PINDA NI MIONGONI MWA MAEFU YA WAKAZI WA MKOA WA KATAVI WALIOSHIRIKI MAPOKEZI HAYO.

WAZIRI MKUU MSTAAFU MIZENGO PINDA AKISALIMIANA NA KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU WA MWAKA 2018 CHARLES KABEHO HAPO JANA MARA BAADA YA MWENGE WA UHURU KUWASIRI MKOANI KATAVI KWA AJIRI YA KUANZA MBIO ZAKE ZA SIKU TANO MKOANI KATAVI PINDA ALIKUWA NI MIONGONI MWA MAEFU YA WATU WAOSHIRIKI MAPOKEZI YA MWENGE ULIOPOKEKEWA KATIKA UWANJA WA NDEGE WA MPANDA UKIWA UNATOKEA MKOANI TABORA ULIOSAFIRISHWA KWA NDEGE KUFUATIA BARABARA INAYOIUNGANISHA MIKOA HIYO KUFUNGWA KUTOKANA NA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA. 
PICHA NA WALTER MGULUCHUMA

MKURUGENZI WA MANISPAA AWAPA ONYO WATENDAJI KWA KUSHINDWA KUTEKELEZA MAAGIZO.

TASAF MANISPAA YA MPANDA IMEANZA UTARATIBU MPYA WA KULIPA WALENGWA KW A NJIA YA MTANDAO.

SERIKALI YA MKOA WA KATAVI YAFUNGA BARABARA YA MPANDA TABORA BAADA YA DARAJA LA MTO KOGA KUJAA MAJI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Mwenyekiti wa wakulima wa tumbaku avamiwa na majambazi na kupolwa

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

KITUO CHA AFYA KANOGE YAKABIDHIWA GARI LA WAGONJWA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Baadhi ya wananchi wa Kata ya Kanoge Makazi ya wakimbizi ya Katumba Wilayani Mpanda Mkoa wakiwa na furaha za kukabidhiwa gari la wagonjwa kwa ajiri ya akina mama wajawazito na watoto lililotolewa na Serikali kwa ajiri ya kituo hicho
Mbunge wa Jimbo la Nsimbo Richald Mbogo akiwa katika gari la wagonjwa lililotolewa na Serikali kwa ajiri ya kituo cha afya Kanoge kwa ajiri ya kububea wajawazito na watoto wadogo gari hilo lilikabidhiwa jana na Mbunge huyo kwa Halmashauri ya Nsimbo Picha na Walter Mguluchuma 



Na  Walter   Mguluchuma.
     Katavi
Kituo cha   Afya  cha   Kanoge  Halmashauri ya  Nsimbo  Wilaya ya  Mpanda   kimekabidhiwa   gari maalumu la  wagonjwa  kwa  ajiri ya  kuwabebea   akina   Mama wajawazito  na  watoto walio na  umri  wa  chini ya   miaka  mitano  ikiwa ni  jitihada  za  Serikali  za  kuokoa uhai wa   Mama  na    mtoto  kufutia kituo  hicho kuwa na tatizo kubwa la  akina  mama kujifungua kwa njia ya upasuaji.
    Gari  hilo  aina ya Zuzuki    lililotolewa na  Serikali   lilikabidhiwa   juzi na   Mbunge wa  Jimbo  la  Nsimbo    Richald  Mbogo  kwa     mganga     mfawidhi wa   kituo cha   afya   Kanoge   Dk   Adamu   Mnyawe    katika   hafla  iliyofanyika  katika    kituo    hicho cha   afya  Kanoge  na  kuhudhuriwa  na  mamia ya  wanachi waliokuwa  wameongozwa na  viongozi wa  Halmashauri ya  Nsimbo .
  Akizungumza  kabla ya  kukabidhi  gari  hilo  la   wagonjwa   Mbunge wa  Jimbo  hilo    Richald   Mbogo    alisema    viongozi  wanatambua  kero  ambazo   zinawakabil  wananchi  na  ndio  maana    Serikali  imetowa    gari  hilo  .
  Alisema  kuw a       Serikali   imetowa  gari  hilo  kwa  kuwa  inatambua   mahitaji   yanayohitajika   kwenye  kituo  hicho cha   afya  na  inaendelea  kuboresha   huduma  za   afya   kwenye kituo  hicho  na   ndio  maana   Serikali  imetowa  kiasi  cha  Tshs 400 ,000,000  kwenye kituo hicho kwa  ajiri ya ujenzi wa  wodi ya  akina   mama ,  chumba  cha  kuhifadhi maiti ,maabara  na  nyumba ya  mganga .
 Aliwataka  waakikishe    gari  hilo  wanalitunza   vizuri   na  kulitumia  kwenye   makusudi yaliyokusudiwa  na  yeye   kama   Mbunge   ataendelea  kuwasemea   Bungeni  wananchi wa  jimbo  hilo juu ya  kero za   afya   zinazowakabili .
Mganga   Mfawidhi wa    kituo   hicho cha  Afya    Dk   Adam  Mnyawe alisema kituo  hicho  cha   afya   cha    Kanoge   kinakabiliwa  na   changamoto  kubwa  ya  akina  mama   wajawazito kushindwa kujifungua  kwa  njia ya  kawaida   hari  ambayo  hulazimu  kuwapatia  rufa     akina      mama  wajawazito  kupekwa  katika   Hospital  ya  Manispaa ya   Mpanda  kutokana  na  kituo  hicho  kutokuwa  na  huduma za upasuaji .
  Alifafanua  kuwa  kwa  mwezi  huwa  wanapokea  wajawazito  kati ya    50 na    60 na wanaoshindwa kujifungua  na  kupewa  rufaa  ya  kwenda  katika  Hospitali ya   Manispaa  huwa  ni  wajawazito kati ya  15  na    18 kwa  kila  mwezi  ambapo  usafirishwa  kwa  kutumia      magari    binafsi  kutokana  na  kituo  hicho  hapo  awali kutokuwa  na  gari     hata  moja .
Nae   Agnes  Nyamalila   Mkazi wa   Kaya   ya  Kanoge    alisema    akina   mama  wajawazito  walikuwa  wakipata shida   sana ya  usafiri  pindi  wanapokuwa  wanashindwa kujifungua  kwa  njia ya  kawaida  hari   ambayo  ilikuwa  ikiwalazimu     wasubilie   usafiri  wa   magari  yanayotoka   Kata ya  jirani ya  Ugala kwa  ajiri ya  kumsafirisha   mjamzito   kwenda   Hospitali ya  Manispaa ya   Mpanda.
Na  kuna  wakati  magari  hayo yalikuwa  hayapiti  hasa   nyakati za  usiku  hari   ambayo  huwalazimu   wanaume  kuwabeba  wagonjwa kwa   kutumia   machela.
Ndaisaba  Jacksoni   alieleza  gari  hilo la  wagonjwa  litawasaidia kupunguza  vifo vya  mama na  mtoto  na  pia  kuwapunguzia  gharama walizokuwa  wakizitumia   ya  fedha  za  kusafirishwa  mjamzitokwani  walikuwa  wakitumia   gharama  kubwa ya  kumsafirisha   kutoka   Kanoge   hadi    Hospitali ya   Manispaa   iliyoko  umbali wa kilometa   30

ASHIKILIWA NA POLISI KWA KUMUUA MKE WAKE NA KUMFUKIA ARDHINI HUKU MTOTO WAKE AKISHUHUDIA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa