Home » » UMBALI WA UPATIKANAJI WA MAJI WASABABISHA WANAWAKE KUPATA KICHAPO KUTOKA KWA WAUME ZAO

UMBALI WA UPATIKANAJI WA MAJI WASABABISHA WANAWAKE KUPATA KICHAPO KUTOKA KWA WAUME ZAO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



Na  Walter  Mguluchuma
     Katavi yetu blog
Baadhi ya  Wanawake   wa  Kijiji  cha  Songambele  Tarafa ya  Nsimbo   Wilaya ya  Mlele   Mkoani  Katavi wamejikuta   katika wakati mgumu  kutokana na kupokea  vipigo  na manyanyaso  mengine  kutoka  kwa waume zao  kutokana  na kutumia  muda  mrefu  katika  kutafuta maji  ambayo ni nitatizo kubwa sana  Kijijini  hapo .
Hayo yalisemwa hapo jana kwa  uchungu  mkubwa   na baadhi ya  Wanawake wa Kijiji  hicho  mbele ya Waandishi wa  Habari waliokuwa wametembelea Kijiji  hicho  katika eneo la kisima cha kutekea maji kilichopo jirani na ofisi za  Halmashauri ya  Nsimbo.
Mmoja wa  akinamama  hao  Maria   Yohana  alisema  baadhi ya  wanawake wa Kijiji  hicho wamekuwa  wakipgwa na waume zao kutoka na  kuchelewa  kupika  chakula kunako sababishwa na foleni kubwa ya kuteka maji inayosababishwa na uhaba wa maji unaokikabili Kijiji  hicho cha  Songa  Mbele .
 Alisema wamekuwa wakilazimika kuamka usiku wa  manane  ili kuweza kuwahi  foleni ya kuteka maji kwa ajiri ya matumizi  mbalimbali ya  nyumbani  maji   hasa  ya kunywa kutoka na kijiji  hicho kuwa kinategemea kisima kimoja tuu.
 Zaluta  Petro  aliwaambia  Waandishi wa Habari  kuwa wamekuwa wakichukua  zaidi ya saa tano  kwa ajiri ya kupanga foleni hadi  inapofika  mtu zamu yake ya kuchota maji kutokana  na kisima  hicho  kuwa na tatizo la  kutotowa  maji  mengi  na  mara  nyingine yamekuwa yakikatika .
 Alisema  wamekuwa wakipata shida  sana kwa wame  wao pindi wanakuwa wamechelewa kutoka kuchota  maji hari ambayo imekuwa ikiwafanya wakati mwingine watuhumiwe na wame zao kuwa walikuwa kwa wanaume wengine kitu ambacho sio  sahihi.
Kwa  upande wake  Cristina  Sabuni   alieleza  kuwa amekuwa akichangazwa na  Halmashauri ya  Nsimbo kutotengeneza kisima   hicho wakati wao  wanapochota  maji  huwa wanalipia kiasi cha  shilingi ishirini kwa kila  ndoo  moja .
Alifafanua  kisima  hicho  pekeekijijini  hapo  kilijengwa  mwaka  1995 kwa msaada wa  aliyekuwa  Mbunge wao ambae  kwa sasa ni  marehemu   Monjor  Sigela  Nsima  tungekuwa na uwezo wa kumfufua  kungefanya  hivyo  alisema   Cristina  kwa masikitiko.
Nae  Stephano  Ally   alieleza  kuwa wameanza kufanya jitihada  wao  kama wakazi wa Kijiji  hicho za kuchangishana   fedha  ili wachimbe kisima kitakacho wasaidia wake zao kuondokana na tatizo la maji.
Mwenyekiti wa  Kijiji   hicho  Beatus  Kambimbaya  alisema    wameisha  iomba  Halmashauri ya  Nsimbo kukifanyia  matengenezo kisima  hicho  ili  maji yaweze kupatikana kwa wingi kwani  ni muda  mrefu sasa kisima   hicho  akijifanyiwa  matengenezo .
  Alisema   ndio maana wakazi  kijiji  hicho wamekuwa  wakiugua mara kwa mara baadhi ya  magonjwa kutokana  na  baadhi yao kutumia  maji ya kwenye   madimbwi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa