Wednesday, January 13, 2016

NAIBU WAZIRI ATOA AGIZO LA KUPIMWA KWA ARDHI ILI KUEPEKA MIGOGORO YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
   Katavi yetu blog
Naibu  Waziri  wa Kilimo uvuvi na ufugaji Wiliamu Ole  Nasha ameuagiza uongozi wa  Serikali wa Mkoa wa Katavi kuhakikisha wanapima wanaweka  mpango bora wa matumizi ya ardhi kwa kupima ardhi na kuitenga kwa ajiri ya matumizi mbalimbali ili kuepukana na migogoro ya mara kwa mara ya Wakulima na wafugaji.
Nasha alitowa agizo hilo hapo jana  wakati alipokuwa akiwatubiwa Wananchi wa Kijiji cha Mwamkulu Wilayani Mpanda kwenye mkutano wa hadhara.
Alisema  migogoro ya ardhi baina ya wakulima na  wafugaji imekuwa ititokea hapa Nchini mara kwa mara kutokana na  kutokuwepo  kwa mipango    bora ya matumizi  ya ardhi kwa  kuitenga kwa ajiri ya matumizi mbalimbali.
Alieleza Serikali ya awamu ya tano imepanga kuhakikisha inashughulikia  na kumaliza migogoro yote ya ardhi  ya wakulima na wafugaji ambayo imekuwa ikiendelea kutokea .
 Alifafanua kuwa Serikali inautegemea sana Mkoa wa Katavi kwa ajiri ya uzalishaji wa mazao ya chakula hivyo  viongozi wa Mkoa huo waakikishe wanaweka mipango  boraya  matumizi ya adrhi kabla ya  haija  haijaalibiwa kwani uongozi wa Mkoa huo wanayonafasi ya kufanya hivyo,
Nasha alisema Mkoa wa Katavi ni Mkoa ambao unapokea watu wengi wanao toka Mikoa ya Kanda ya Ziwa  wanao hamia hapo kwa ajiri ya  kufanya shughuli  za ufugaji na kilimo hivyo wasipokuwa na mipango mizuri ya matumizi bora ya ardhi upo uwezekano mkubwa wa kuharibika kwa ardhi ,
Pia ameutaka uongozi wa Serikali kuhakikisha watu wanao hamia Mkoani hapo hawahamii kiholela bali wahamie kwa kufuata  utaratibu wa sheria .
 Naibu Waziri  Nasha  vilevile  amewataka watendaji wa Serikali  kufanya kazi kwa bidii na kwa uadilifu  mkubwa  kwani  Serikali imepanga kuwa karibu na wananchi kwa kusikiliza na kushughulikia  na kutatua kero  za wananchi  hivyo watendaji waache kukaa  ofisini bali waende kusikiliza kero za wananchi.
Alisema Serikali imejipanga  kuhakikisha  pembejeo za kilimo  zinamfikia mkulima kwa  wakati na  inamchulia hatua mtu yoyoye ambae atasababisha pembejeo zishindwe kufika kwa wakati kwa mkulima .
Nae  Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Madeni Kipande  alimwakikishia Naibu Waziri kuwa  Mkoa huo utaanza kutekeleza agizo  la  upimaji wa ardhi  kwa ajiri ya  mipango bora ya matumizi bora ya ardhi   kwa kutumia fedha zao za makusanyo ya ndani bila kusubilia  fedha za kutoka Serikali kuu kwani jambo hilo walalichukulia kwa umuhimu mkubwa.
Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima  alieleza kuwa watu wamekuwa wakihamia Mkoani Katavi kutokana na Mkoa huo kuwa na ardhi kubwa .
Alisema  Mkoa huo ndio  Mkoa pekee kwa sasa  ambao ardhi yake ni yenye rutuba nzuri  na ambayo haija alibiwa .
Naibu Waziri Nasha amemaliza ziara yake ya siku tatu ambayo ilikuwa na lengo la kuhamasisha maendeleo na kushughulikia malalamiko ya wakulima wa Tumbaku wa vyama vya ushirika wa Tumbaku vya  Mpanda Kati na Ukonongo .

No comments:

Post a Comment