Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi yetu blog
Zaidi ya Ekari
1,200 za ardhi za maeneo tengefu
zimeharibiwa Wilayani Mpanda Mkoani Katavi kutokana na watu
kufanyia shughuli za kibinadamu
na ufugaji wa mifugo
Mkuu wa Wilaya ya
Mpanda Paza Mwamlima alieleza hayo hapo jana mbele ya waandishi wa habari ofisini kwake
wakati alipokuwa akitowa taarifa za
shughuli zilizo tekelezwa na
Serikali ya Wilaya ya Mpanda kwa kipindi cha mwezi mmoja
Alisema jumla ya ekari 1,240 za maeneo tengefu ya ardhi zimaharibiwa
Wilaya Mpanda kutokana na watu
kuvamia maeneo hayo na kufanya shughuli za kibinadamu
Alitaja sababu ya maeneo hayo kuharibiwa kuwa ni watu kufanya shughuli
za kilimo kujenga makazi ya
kuishi na kufanyia shughuli za ufugaji wa mifugo ya aina mbambali
Alisema
kutokana na uharibifu huo Wilaya imejipanga kuhakikisha maeneo hayo yaliharibiwa yanarudia katika
hari yake ya kawaida na pia maeneo
mengine yasiharibiwe
Alifafanua
kuwa kutokana na hari hiyo ya uharibifu
wa maeneo tengefu ya ardhi wameanza
kuchukua hatua mbalimbali za kukabiliana
na tatizo hilo
Mwamlima alizitaja hatua walizochukua ni kuwaondoa
wavamizi waliovamia misitu
na wamewakamata na wamewafikisha
mahakamani
Pia wameharibu vibanda vyote vilivyomo ndani ya misitu na wamekamata Ng’ombe na kutoza faini
na kisha wameziondoa katika misitu
ya Mkoa wa Katavi
Alisema Wilaya ya Mpanda imeweka utaratibu
wa kudhibiti uvamizi wa maeneo
ya hifadhi unaofanywa kwa kuweka
makazi ,kilimo kuchungia
mifugo ujangiri wa wanyama pori
na uvunaji wa magogo hususani
katika maeneo ya msitu
wa hifadhi wa Tongwe mashariki
,Nkamba na ushoroba
wa wanyamapori wa Lyamgoroka na misitu
hifadhi ya vijiji vya Mpembe na
Katuma
No comments:
Post a Comment