Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi yetu blog
Hari ya Chama cha Demokrasia (Chadema)
Mkoani katavi si shwari hari iliyopelekea viongozi wa
Chama hicho wa ngazi ya Mkoa na Wilaya
kusimamishwa uongozi kwa
kutuhumiwa kukisaliti Chama hicho wakati
wa uchaguzi mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu
Viongozi hao walisimamishwa uongozi hapo juzi katika mkutano wa kamati ya mashauliano ya chama hicho uliofanyika katika ukumbi wa Katavi Resort Mjini hapa na ulitawaliwa na vurugu
kubwa ya wafuasi na wanachama waliokuwa wakishinikiza
viongozi wao wajiuzuru
Viongozi
waliosimamishwa na mkutano huo uliongozwa na
mtaribu wa Chadema wa Kanda ya Magharibi
Cristophar Namwanji ni Katibu wa
Bawacha Hamisa Korongo wa
Mkoa na Mwenyekiti wa Bavicha
Fransis Misigaro
Viongozi wengine waliosimishwa ni
Mwenyekiti wa Chadema wa Wilaya
ya Mpanda Abrahamu Mapunda na
katibu wa Wilaya Idd Faraji pamoja na
Mwenyekiti wa Bavicha na Katibu wa
Bawacha wa Wilaya ya Mpanda
Mkutano huo pia
umewasimamisha uongozi viongozi wa jimbo
la Mpanda Mjini ambao ni Mwenyekiti wa Jimbo la Mpanda Mjini Braisoni Mwalugala Katibu wa Jimbo hilo Patrick Richald na
Katibu na Mwenyekiti wa jimbo wa Bavicha
na Bawacha
Viongozi hao
waliosimamishwa wanadaiwa kuwa walikiujumu chama hicho wakati wa uchaguzi mkuu na kusababisha chama
hicho kushindwa vibaya wakati wa
uchaguzi mkuu uliofanyika hivi karibuni
na kupoteza jimbo la Mpanda Mjini
liliokuwa lililoongozwa na Said
Arfi(Chadema) kwa kipindi cha miaka kumi
Mbali ya
kusimamishwa uongozi viongozi hao wametakiwa kukabidhi mali zote za Chama hicho zikiwemo pikipiki walizokuwa
wakizitumia kufanyia shughuli za chama hicho
Mkutano huo ulifanyika
huku kukiwa na ulinzi mkali wa polisi waliokuwa wamevaa sare na wengine wasio na sare wakiwa wameongozwa na mkuu wa Kituo kikuu cha Polisi cha Wilaya ya Mpanda
kufuatilia kuwepo kwa dalili za kuwepo kwa vurugu kwenye mkutano huo
Hivi
karibuni wafuasi na wanachama
wa chama hicho walivamia ofisi za Mkoa
kwa lengo la kuwashinikiza
viongozi hao wajiuzuru kutokana na
kukiujumu chama hicho
Kwa upande wake
katibu wa Chama hicho wa Wilaya ya Mpanda Idd Faraji
alisema kuwa mkutano huo haokuwa
halali kwani wajumbe
walioshiriki kutowa maamuzi hayo
hawakuwa ni wajumbe halali wa mkutano
huo
No comments:
Post a Comment