Tuesday, June 2, 2015

HATARII! AJINYONGA BAADA YA KUKATILI WA KUWEKWA MAHABUSU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na  Walter  Mguluchuma
Katavi  
Mtu mmoja  aliyefahamika kwa jina  la Petro  Magawe (40) Mkazi wa  Mtaa wa Ilembo  Wilaya ya Mpanda  amekutwa  akiwa  amejinyonga  kwenye mti  kwa kutumia  shati lake  alilokuwa amevaa
 Kamanda wa Polisi wa Mkoa  wa Katavi kamishina mwandamizi msaidizi Dhahiri Kidavashari aliwaambia waandishi wa Habari jana kuwa tukio hilo la kujinyonga kwa mtu huyo lilitokea hapo jana majira ya saa mbili asubuhi  katika eneo la ofisi ya mistu  katika mtaa wa Majengo A  mjini  hapa
 Kabla ya tukio hilo   marehemu huyo alifika kwenye  kituo cha Polisi  cha Wilaya ya Mpanda  nakueleza  kuwa  anaomba  na anahitaji awekwe  mahabusu
 Kamanda Kidavashari alisema  kauli hiyo ya marehemu aliyoitowa ya kuomba  awekwe mahabusu iliwashitua polisi waliokuwa zamu kwani sio jambo la kawaida kwa mtu kuomba awekwe mahabusu
 Hivyo  marehemu alipatiwa msaada  wa kupewa PF 3 kwa ajiri  ya kwenda Hospitali  kupatiwa matibabu kwani alionekana  kama mtu aliyechanganikiwa
 Kamanda Kidavashari alisema  baada ya marehemu kuwa amepewa PF 3  alioga kwenye kituo cha polisi kuwa anaelekea hospitalini
 Alieleza  baada ya hapo  marehemu alikuja kuonekana hapo jana  majira ya saa kumi na mbili asubuhi  akiwa amejinyonga juu ya mti kwa kutumia  shati lake
 Kidavashari alisema chanzo cha tukio  hilo bado haki  kulikana  na jeshi la polisi  linaendelea  na uchunguzi  wa tukio hilo

No comments:

Post a Comment