Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter Mguluchuma
Katavi yetu blog
Watu wawili wa familia moja Mke na Mume wakazi wa Kitongoji cha Makambo Kata ya Itenka Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wameuwawa kikatili kwa kuchinjwa shingo zao na kutenganishwa na kiwiliwili wakati wakiwa wamelele ndani ya nyumba yao na watu wasiofahamika
Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwataja wanandoa hao wawili waliouwawa kikatili kuwa ni Seth Mwakalimbwa (65) na Yakoba Kalulu(48) wakazi wa kitongoji hicho
Kidavashari aliwaambia jana waandishi wa habari kuwa tukio hilo la mauwaji ya kikatili lilitokea hapo juzi majira ya usiku nyumbani kwa wanandoa hao waliokuwa wakiishi pamoja kama mke na mume
Alisema kwamba marehemu hawa wakati wa uhai wao walikuwa wakiishi kwenye nyumba yao huku wakiwa p eke yao pasipo kuwa na watu wengine kwenye nyumba hiyo waliishi kwa muda mrefu
Ilipo fika juzi asubuhi balozi wa eneo hilo aitwaye Wilbroad Mahenge ambae ni jirani ya marehemu hao aliingiwa na mashaka baada ya kutowaona wanandoa hao wawili kwa kipindi cha siku mbili mfululizo
Kamanda Kidavashari alieleza balozi huyo kutokana na kutowaona wanandoa hao aliamua kufika katika makazi yao na alipofika hapo alikuta mirango ya nyumba yao aliikuwa iko wazi hari ambayo ilimfanya apate mashaka zaidi
Alisema alijaribu kuwaita kwa majina yao lakini hakuna aliyeweza kuitika na aliamua kuingia ndani ya nyumba yao na ndipo aliwakuta wakiwa wamelazwa kitandani huku wakiwa wamefariki dunia kwa kuchinjwa shingo zao na kutenganishwa na kiwiliwili
Baada ya kuona hari hiyo balozi Wilbroad alitoka nje na kasha alikwenda kutowa taarifa kwenye uwongozi wa Serikali ya Kitongoji ambao na wao walitowa taatifa kwa jeshi la polisi ambao walifika kwenye eneo hilo baada ya muda mfupi
Kamanda Kidavashari alisema chanzo cha tukio la mauwaji hayo ya kikatili linahusishwa na imani za kishirikina na mpaka sasa hakuna mtu wala watu waliokamatwa kuhusika na tukio hilo
Aidha jeshi la polisi kwa kushirikiana na uongozi na wanakijiji cha Makambo wanaendelea na msako ili kuweza kuwabaini wale watu wote waliohusika katika mauwaji ya wanandoa hao
Katavi yetu blog
Watu wawili wa familia moja Mke na Mume wakazi wa Kitongoji cha Makambo Kata ya Itenka Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi wameuwawa kikatili kwa kuchinjwa shingo zao na kutenganishwa na kiwiliwili wakati wakiwa wamelele ndani ya nyumba yao na watu wasiofahamika
Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari aliwataja wanandoa hao wawili waliouwawa kikatili kuwa ni Seth Mwakalimbwa (65) na Yakoba Kalulu(48) wakazi wa kitongoji hicho
Kidavashari aliwaambia jana waandishi wa habari kuwa tukio hilo la mauwaji ya kikatili lilitokea hapo juzi majira ya usiku nyumbani kwa wanandoa hao waliokuwa wakiishi pamoja kama mke na mume
Alisema kwamba marehemu hawa wakati wa uhai wao walikuwa wakiishi kwenye nyumba yao huku wakiwa p eke yao pasipo kuwa na watu wengine kwenye nyumba hiyo waliishi kwa muda mrefu
Ilipo fika juzi asubuhi balozi wa eneo hilo aitwaye Wilbroad Mahenge ambae ni jirani ya marehemu hao aliingiwa na mashaka baada ya kutowaona wanandoa hao wawili kwa kipindi cha siku mbili mfululizo
Kamanda Kidavashari alieleza balozi huyo kutokana na kutowaona wanandoa hao aliamua kufika katika makazi yao na alipofika hapo alikuta mirango ya nyumba yao aliikuwa iko wazi hari ambayo ilimfanya apate mashaka zaidi
Alisema alijaribu kuwaita kwa majina yao lakini hakuna aliyeweza kuitika na aliamua kuingia ndani ya nyumba yao na ndipo aliwakuta wakiwa wamelazwa kitandani huku wakiwa wamefariki dunia kwa kuchinjwa shingo zao na kutenganishwa na kiwiliwili
Baada ya kuona hari hiyo balozi Wilbroad alitoka nje na kasha alikwenda kutowa taarifa kwenye uwongozi wa Serikali ya Kitongoji ambao na wao walitowa taatifa kwa jeshi la polisi ambao walifika kwenye eneo hilo baada ya muda mfupi
Kamanda Kidavashari alisema chanzo cha tukio la mauwaji hayo ya kikatili linahusishwa na imani za kishirikina na mpaka sasa hakuna mtu wala watu waliokamatwa kuhusika na tukio hilo
Aidha jeshi la polisi kwa kushirikiana na uongozi na wanakijiji cha Makambo wanaendelea na msako ili kuweza kuwabaini wale watu wote waliohusika katika mauwaji ya wanandoa hao
No comments:
Post a Comment