Na Walter
Mguluchuma
Katavi yetu blog
Mkoa wa
Katavi unakabiliwa na changamoto
kubwa la
kuwa na barabara za udongo
ambazo huharibika kipindi
cha masika na kusababisha usumbufu
mkubwa kwa wakazi wa Mkoa huo
Hayo yalielezwa hapo juzi na Kaimu Mkuu wa
Mkoa wa Katavi ambae pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima wakati
alikuwa akisoma taarifa ya sekta ya
Barabara ya Mkoa wa Katavi mbele ya Waziri wa ujenzi Dr John Magufuli
kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika
kwenye uwanja wa shule ya Msingi Mpada mjini hapa
Alisema
mtandao wa barabara katika Mkoa
wa Katavi bado
hauko imara kwani
barabara nyingi za Mkoa wa Katavi ni za shangalawe na udongo ambazo huaribika mara
kwa mara hasa kipindi cha masika
Alifafanua
kuwa Mkoa wa Katavi unajumla
ya kilmeta 1,101.46 za barabara zinazohudumiwa na wakala wa
Barabara wa Mkoa TANROADS kati ya hizo kilometa 473.3 ni barabara kuu na kilometa 627 .16 ni barabara za Mikoa
Hata hivyo
kupitia wakala wa barabara Mkoa wa Katavi hadi sasa
angalau kuna barabara mbili zinazojengwa kwa kiwango cha rami
Barabara hizo
alizitaja kuwa ni barabara ya
Kateto kwenda Kibaoni yenye
urefu wa kilometa 20.27 na barabara
ya Sitalike kwenda Mpanda yenye urefu wa kilometa 36.90
Alisema
Mkoa unatarajia kuipa
kipaumbele Mikoa ya pembezoni
mwa nchi ukiwemo Mkoa wa
Katavi ilikuweza kurahisisha
huduma za maendeleo kwa kuiunganisha na Mikoa
mingine kwa barabara bora za lami
Muelekeo wa Mkoa wa Katavi sasa ni kuelekea
katika uchumi wa Nishati ya mafuta na
Gesi na utafiti unaendelea Ziwa Tanganyika hivyo suala la mtandao wa bora wa barabara za
lami ndani ya Mkoa na Mikoa ya jirani linatakiwa kupewa kipaumbele cha hari ya juu kwani
kuufungua mkoa wa Katavi ni
kuifungua Tanzania na kanda nzima ya Maziwa Makuu
ikiwemo nchi ya DRC Congo
Kwa upande wake Dr John Magufuli alieleza kuwa
Serikali inatajia kumpatia kiasi
cha shilingi Bilioni 1.3 mkandarasi anaetengeneza barabara ya lami Sitalike Mpanda iliaweze kumaizia ujenzi wa barabara
hiyo ambayo tayari kilomete 26
zimekamilika
Mkandarasi
anaetengeneza barabara ya Kateto kwenda Kibaoni hari ya ujenzi wa barabara hiyo inayojengwa
na kampuni ya Kichina bado hairidhishi
na ametakiwa amalize ujenzi wa barabara hiyo kwa muda alipangiwa
vinginevyo atafutiwa mkataba wake alisema Dr Magufuli
Alieleza Serikali itatoa kiasi cha shilingi milioni 600 kwa ajiri ya matengenezo ya baraba kwa
kiwango cha changalawe kutoka sitalike
kwenda kibaoni yenye urefu wa kilometa 70 pia
Serikali inatarajia kuzipatia Halmashauri za Mji wa Mpanda na
Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda kiasi cha shilingi Bilioni 1.6 kwa ujenzi wa
barabara za Halmashauri hiyo
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
No comments:
Post a Comment