Friday, January 30, 2015

WAKURUGENZI WATAKIWA KUWA NA UTARATIBU WA KUKUTANA NA WAALIMU ILIKUSIKILIZA KERO ZAO


Na  Walter  Mguluchuma
Katavi yetu blog
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dr  Ibrahimu Msengi amewataka Wakurugenzi watendaji   na maafisa Elimu wa Halmashauri zote za Mkoa wa Katavi kuwa na utaratibu wa kukutana na waalimu ili  kuwasililiza matatizo yao  yanayowabili  Waalimu
Dr  Msengi alitowa wito huo hapo juzi wakati alipokuwa akizungumza na waalimu  wa shule za misingi na Sekondari walioko kwenye makazi ya Wakimbizi ya Mishamo  kwenye mkutano uliofanyika katika shule ya Sekondari ya Mishamo wakati wa ziara yake ya kukagua  ujenzi wa majengo ya maabara kwenye Sekondari ya Mishamo
 Alisema nilazima Wakurugenzi  watendaji wa Halmashauri na maafisa elimu  watengeneze mfumo ambao utawafanya  waweze kuwa wanakutana na waalimu  na kuwasikiliza matatizo yao
 Alifafanua tabia ya viongozi  kutokutana na waalimu na kuwasikiliza  kumewafanya waalimu  kutumia muda mwingi kwenda kwenye ofisi za Halmashauri  kufuatilia madai yao mbalimbali
 Alisema   hari   hiyo imekuwa ikiwafanya waalimu kutumia muda  mchache kuwafundisha wanafunzi kutona na kutumia muda mwingi kufuatilia madai yao
Pia alieleza  Halmashauri  waandae  mfumo utakao  wafanya waalimu  wahudumiwe  mapema iliwawze  kurudi mapema kwenye shule zao  na kuwafundisha masomo wanafunzi
 Dr  Msengi alieleza  endapo waalimu watahudumiwa shida zao na mapema  itawafanya  waendelee  kuwa na moyo wa kufanya kazi zaidi  kutokana na wao kuonawanathaminiwa
 Alisema itashangaa kuona mwalimu  inashindwa kuhudumiwa kwa wakati  wakati  maafisa Elimu na wao ni waalimu wenzao na matatizo ya waalimu wanayafahamu hivyo hawapaswi kusahau waliko toka na watambue kuwa maafisa Elimu na wao ni waalimu
Aidha kuhusu matatizo ya nyumba za waalimu alisema Mkoa  unaandaa utaratibu wa kuanzisha mfuko maalumu kwa ajiri ya ujenzi wa  nyumba za waalimu kwa kuwashilikisha wadau mbalimbali mbapo  kila mwaka watakuwa wanaweza kujenga nyumba  mbili za waalimu kila shule kwa kila mwaka
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

No comments:

Post a Comment