Monday, July 28, 2014

HALMASHAURI YA NSIMBO YAVUKA LENGO LA KUKUSANYA MAPATO

Jiunge na Huduma ya Tone Mobile News Bure kabisa kupitia Whatsapp yako na uwe wa kwanza kupata kile kinachotokea ni Rahisi sana Ingia katika uwanja wa kuandika ujumbe mfupi wa maneno katika Whatsapp yako kisha andika TONE MOBILE NEWS tuma kwenye namba 0756364660 utapokea ujumbe kuwa umeunganishwa.

Na  Walter  Mguluchuma
Mpanda Katavi
 Halmashauri ya Wilaya  ya Nsimbo  Mkoani  Katavi imefanikiwa  kukusanya mapato ya ushuru  wa ndani  jumla ya shilingi Tsh  753,042,184 kwa  kipindi cha  june 2013 hadi june 2014 ikiwa ni asimia 105.6 ya lengo la makusanya  waliokuwa wamepanga kukusanya
Hayo yalisemwa hapo jana na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nsimbo  Neneka Rashid  wakati wa  Mkutano mkuu wa Baraza la Madiwani wa Halmashauri   ya  Nsimbo  uliofanyika  katika ukumbi wa Hakmashauri  hiyo
Rashid  alisema  Halmshauri  hiyo  ilikuwa  imeweka  lengo la  kukusanya mapato ya Tsh  713,328,000 lakini  imeweza  kuvuka  lengo kwa kukusanya kiasi cha  Tsh  753,042,184  ambazo ni sawa  na  asilimia  105.6
Alifafanua  kutokana na kukusanya kiwango hicho  cha mapato  ya  ndani Halmashauri  hiyo imewaza  kuvuka lengo walilokuwa wamepanga kwa  kiwango  cha asilimia  5.6
Alitaja  sababu zilizofanya  Halmashauri hiyo kuvuka lengo la makufanyo kuwa  Halmshauri iligawanya  vyanzo  vya mapato  yaani  mazao ya kilimo  na magulio  kwa eneo moja
 Pia  walifanya  ukaguzi wa mara kwa mara wa kuwakagua mawakala  na waliweza kutoa maelekezo kwa mawakala  pale palipohitajika na mawakala  walifuata maelekezo  hayo
Alisema  Halmashauri  imefanikiwa  kuweza kujibu  hoja zote za ukaguzi wa ndani na za nje  imeweza  kuzijibu kwa wakati  pale  walipotakiwa kufanya hivyo
Rashid  alitaja baadhi ya  changamoto zinazokabili  Halmashauri hiyo kuwa ni  migogoro  ya mara kwa mara  baina ya Madiwani  na watendaji wa Halmashauri
Changamoto nyingine   ni watendaji wa vijiji  na  Kata kutoitisha vikao vya kikatiba kwenye maeneo yao na kusababisha wananchi kutosomewa  mapato na matumizi  na kuwafanya wananchi kutokuwa na imani  na viongozi hao na kuwavunja moyo wananchi wa kujitokeza kwenye shughuli za kujitolea
Kwa upande wake  Diwani wa Kata ya  Machimboni   Raphael Kalinga  aliomba  Halmshauri  hiyo  iwe inaweka wazi mikataba ya wakandarasa kwenye eneo la mradi husika kwani mikataba mingi imekuwa  ni yasiri
Alisema endapo mikataba itakuwa wazi kwa  madiwani itawafanya waweze kuisimimia miradi inayojengwa kwenye kata zao kwa ukalibu zaidi
 Nae  afisa   wa  Serikali wa Mitaa wa Mkoa wa Katavi Lauteri Kanoni aliita Halmashauri hiyo kuendelea kubuni  mapato mengine yatakayoiongezea  Halmashauri ya Nsimbo mapato yao
Alieleza  utaratibu  wa kukusanya mapato  unaweza kubadilika wakati wowote kwani  baadhi ya mapato yanaweza yakabadilishiwa utaratibu  badala ya kukusanya na Halmashauri yakakusanywa na Serikali kuu  hivyo wasitegemee sana ushuru wa zao la Tumbaku  ambao ndio  unaoingiza ushuru mkubwa kwenye Halmashauri hiyo
Alisema   katika Halmashauri  nne zilizopo   katika  Mkoa  wa Katavi ni Halmashauri mbili ambazo zimeweza kuvuka  lengo la ukusanyaji wa  mapato ya ndani alizitaja   Halmashauri hizo kuwa ni  Nsimbo  na Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

No comments:

Post a Comment