Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Mpanda Katavi
Tume ya
uchaguzi imeongeza vituo vya
kuandikisha vya kupigia kura
katika uboreshaji wa daftari la wapiga kura kutoka vituo
24,919 hadi kufikia vituo 40,015
Haya yalisemwa
hapo juzi na Kamishina wa Tume ya Taifa ya uchaguzi Prof
Amon Chaligha wakati
akifungua kikao cha tume ya
Taifa ya uchaguzi na waandishi wa habari wa
Mkoa wa Katavi kilichofanyika
kwenye ukumbi wa Idara ya Maji mjini hapa
Alisema tume ya uchaguzi inatarajia
kufanya uboreshaji wa Daftari la kudumu
la wapiga kwa awamu ya kwanza
hivi karibuni kwa kutumia Teknolojia
mpya ya Blometric voter Registration(BVR)kwa ajiri ya uchaguzi mkuu
wa mwaka 2015
Alifafanua uandikishaji wa sasa utafanyika katika
vituo vilivyo katika ngazi ya Vitongoji
Vijijin na mitaa tofauti na ilivyo kuwa
huko nyuma
Prof
Chaligha alieleza uandikishaji wa huko awali ulikuwa ukifanyika kwenye ngazi ya Kata
hivyo kwa utaratibu wa sasa
vituo vya kujiandikishia vimeongezeka
kutoka 24,919 na kufikia 40,015
Lengo la
kuongeza vituo ni kuwawezesha watu kuwa
karibu zaidi na vituo vya kujiandikishia na hivyo itapunguza malalamiko
ya wananchi ya kulalamikia kuwa
vituo viko mbali na wanako ishi
Alisema Tume ya
uchaguzi kwa kuongeza vituo na
kuvisogeza karibu na wannchi
wanayomatumaini wajiandikishaji wataongezeka
na mwamko wa kupiga kura utakuwa
ni mkubwa

No comments:
Post a Comment