Na Walter Mguluchuma
Zaidi ya Wakazi elfu moja wa Kijiji cha Sungamila Kata ya
Kasokola Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi watanufaika na mradi wa maji
unaofadhiliwa na Benki ya Dunia
mradi ambao utagharimu
shilingi milioni mia mbili
Hayo yamelezwa na
Diwani wa Kata ya Kasokola Crisanti
Mwanawima hapo jana wakati akizungumza
na mwandishi wa habari kwenye
ofisi yake ya Kata iliyopo katika
Kijiji cha Kasokola
Alisema kijiji
hicho chenye jumla ya wakazi elfu moja
na miambili wanatarajiwa kunufaika na
mradi huo unaogharamiwa na Benki ya
Dunia kwa gharama ya shilingi milini
miambili unatarajiwa kukamilika hapo mwakani
Alifafanua kuwa
mradi huo ulianza hapo mwaka 2011 kwa
hatua ya uchimbaji wa mitalo ya kuwekea mbomba
na mwezi ujao shughuli ya ujenzi
wa tanki la kuhifadhi maji unatarajiwa kuanza mwezi ujao
Mwanawima
alisema mradi huo utakapokuwa
umekamilika utasaidia kuondoa tatizo la maji Kijijini hapo kwani Kijiji
hicho kinakabiliwa na tatizo la uhaba wa maji kwani kijiji hicho
kina visima vifupi viwili tuu vinavyo towa huduma ya maji kwa wakazi
wa Kijiji cha Sungamila
Alisema lengo la mradi huo utakapo kuwa umekamilika ni kusambaza
maji kwenye baadhi ya vijiji
vinavyo zunguka Kijiji cha
Sungamila kutokana na kiwango kikubwa
cha maji kitakacho kuwa kinapatikana
Mbali ya Kijiji hicho pia vijiji viwili vilivyopo kwenye
Halmashauri ya Nsimbo Wlaya ya Mlele navyo vitanufaika na mradi kama huu unaofadhiliwa
na Benki ya Dunia vijiji hivyo ni Kapalala
na Isinde
No comments:
Post a Comment