Na Walter
Mguluchuma
Mpanda Katavi
Mtu mmoja
aliyefahamika kwa jina la Michael
Silanda (26 ) Mkazi wa
Kijiji cha Ibindi Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi amefariki
Dunia baada ya kunywa Pombe (VIROBA ) aina ya Zed
kupita kiasi bila kula
Kwa mujibu wa
Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa Kamishina msaidizi mwandamizi
Dhahiri Kidavashari tukio hilo
lilitokea hapo mei tano mwaka huu majira
ya saa sita usiku kijijini hapo
Alisema siiku hiyo ya
tukio marehemu baada ya
kuamka asubuhi nyumbani kwake hapo majira ya saa tano asubuhi
alielekea kwenye Bar ambayo ilikuwa ikiuza vinywaji vya aina mbalimbali vya pombe kali
na vinywaji baridi
Alifafanua kuwa
baada ya kufika kwenye Bar hiyo aliwakuta
baadhi ya wanakijiji wenzake
wakiwa wanakunywa pombe za aina
mbalimbali hari ambayo ilimfanya
marehemu aweze kujumuika nao kwa kuagiza pombe (VIROBA ) aina ya Zed
Alisema Michael
aliendelea kunywa viroba
kuanzia muda huo kwenye bar hiyo bila kula kitu chochote hadi
hapo majira ya saa sita usiku
alipoamua kurudi nyumbani kwake
huku akiwa amelewa pombe kupita kiasi
Baada ya kufika
nyumbani kwake aliingia ndani ya nyumba yake
na kulala bila kula chakula chochote
na siku iliyofuata majira ya saa mbili asubuhi ndipo
walipomkuta Michael akiwa
amefariki Dunia huku akiwa amelala kitandani kwake
Kamanda
Kidavashari alisema uchunguzi wa awali oliofanywa
kuhusiana na kifo hicho umebaini kuwa kifo hicho kimesababishwa na marehemu kunywa pombe nyingi kupita
kiasi bila kula chakula
Alisema mwili wa marehemu Michae Silanda umehifadhiwa
kwenye chumba cha kuifadhi maiti katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa ajiri
ya kufanyiwa uchunguzi wa Kidaktari na
baada ya uchunguzi huo watakabidhiwa ndugu wa marehemu kwa ajiri ya utaratibu wa mazishi
No comments:
Post a Comment