Friday, May 30, 2014

MBARONI KWA KUKAMATWA NA NOTI BANDIA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma   
Mpanda Katavi
Jeshi la Polisi Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi linamshikilia  Shabani  Hamad (48) Mkazi  wa Mtaa wa Mpanda Hoteli mjini  hapa kwa kutuhumiwa  kukamatwa na fedha  noti bandia kiasi cha shilingi laki moja
Kamanda wa Jeshi la Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari alisema mtuhumiwa  Shaban alikamatwa na fedha  hizo noti  bandia hapo Mei  24  mwaka huu majira ya saa kumi jioni katika eneo la Mtaa wa Mpanda hoteli Mjini  hapa
Mtuhumiwa huyo kabla ya kukamatwa   siku moja  kabla ya tukio hilo la kukamatwa  yaani mei 23  alikwenda kwenye kibanda kinachotowa huduma ya M-PESA  kilichoko  katika  mtaa wa Kawajense na alimkuta muhudumu wa kibanda  aitwaye  Maria Joseph  na kumuomba ampatie huduma ya kuweka fedha kiasi cha shilingi laki moja kwenye simu yake  mkononi
Kidavashari alifafanua  baada ya  mtuhumiwa  Shabani  kukabidhi kiasi hicho cha fedha  kiasi cha shilingi laki moja za noti za shilingi elfu mbilimbili mhudumu wa  kidanda hicho alimwingizia fedha kwenye  akaunti ya simu yake na kisha mtuhumiwa aliondoka kwenye eneo hilo
Alisema  mara baada ya muda mfupi mhudumu wa kibanda alianza kuzipanga fedha  hizo na ndipo aliposhituka  alipoona namba  za noti hizo  zinafana hari ambayo ilimfanya  awape taarifa wafanya biashara wenzake waliokuwa kwenye eneo hilo na juhudi za kumsaka mtuhumiwa zikaanza hata hivyo hawakuweza kufanikiwakumpata  kwani mtuhumiwa alikuwa ametokomea kusiko julikana
Alieleza ndipo mhudumu wa kibanda hicho cha M-PESA alipoamua kwenda kutowa taarifa kwa jeshi la polisi  kituo cha  Wilaya ya Mpanda  kuhusiana na tukio hilo
Baada ya taarifa hizo jeshi la polisi lilianza  msako  wa  kumtafuta mtuhumiwa  ambapo waliweza kufanikiwa  kumkamata mtuhumiwa akiwa katika eneo la mtaa wa mpanda hoteli akiwa na notinyingine  bandia  za shilingi elfu  mbili mbili  zenye thamani ya shilingi laki moja ambazo alikuwa amezichanganya na noti nyingine ambazo ni harali  
Kamanda Kidavashari  alieleza  kuwa Mtuhumiwa alikamatwa nabaadhi  ya  noti hizo  bandia zenye  namba CK 194915  noti 20  Ck 1942911 noti 9 Ck 1942955 noti 11
Mtuhumiwa anatarajiwa  kufikishwa mahakamani wakati wowote mara baada ya kukamilika kwa uchunguzi wa kuhusiana  na tukio hili
kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi ametowa wito kwa wananchi wa Mkoa huu  kujiadhari na matapeli wanaozagaza noti  bandia hasa katika kipindi hiki cha mavuno   na mauzo ya mazao mbalimbali

No comments:

Post a Comment