Friday, March 7, 2014

HOT NEWS: JELA KIFUNGO CHA MIAKA 30 KWA KOSA LA KUMLAWITI KIJANA MWENZAKE BAADA YA KUMYWESHA POMBE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na  Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Mkoa wa Katavi imemuhukumu  Wiliamu  George 32 Mkazi wa Mtaa wa Nsemlwa  Wilaya ya Mpanda  kifungo cha miaka  30  jela baada ya kupatikana na hatia ya kumlawiti  kijana mwenzie  22 Mkazi wa Mtaa wa Mpandahoteli baada ya kumnywesha pombe ya kienyeji kupita kiasi
Hukumu  hiyo  ilitolewa  hapo  jana  na  Hakimu  mkazi   mfawidhi wa  Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga  Ntengwa   nahukumu  hiyo   kuvuita hisia za watu mbalimbali  wa  maeneo ya mjiwa Mpanda na Mkoa wa Katavi
Hukumu  hiyo ilitolewa na Hakimu wa mahakama hiyo  baada ya  mahakama  kuridhika  na  ushahidi  uliotolewa  mahakamani hapo wa   upande wa mashitaka na upande wa utetezi
Katika kesi hiyohapo awali mwendesha mashita mkaguzi wa jeshi la polisi Ally Mbwijo  alidai mahakamani hapo kuwa  mshitakiwa  alitenda kosa hilo hapo Novemba  21 mwaka jana   majira ya kumi na mbili jioni  katika mtaa wa Mpanda Hotel
Mshitakiwa  siku  hiyo ya tukiokabla ya kutenda  kosa  hilo la kumlawiti kijana  huyo alidaiwa  kunywesha pombe  ya kienyeji aina ya komoni  walikuwa wakichanganya na bia  nyumbani kwa mwamke  aliyekuwa akiwauzia pombe aliyetambulika kwa jina moja la Lita katika mtaa huo wa Mpanda hotel
Ilielezwa na mwendesha mashita Ally Mbwijo  kuwa  mshitakiwa  baada ya kuona mwenzake  ametoka  anatoka njekwenda kujisaidia  alimwagiza dukani  Lita  aende akamnulie  sigara
Aliileza mahakama baada ya  kijana  huyo ambaejina lake limehifadhiwa  kurudi  ndani  aliendelea na kunywa pombe ambayo alikuwa ameisha kwenye chupa yake na  ndipo alipoteza fahamu na mshitakiwa alitumia nafasi huyo kumwingilia  kinyume cha maumbile yakehuku akiwa amemlaza kwenye kochi
Mwendesha  mashita  alieleza  Lita  alipotoka  dukani  alimkuta  mshitakiwa akiwa amekaa karibu na kijana huyo  ambae alikuwa  amevuliwa nguo yake  ya saruali  na akiwa akitambui na sehemu zake za  matakoni zikiwa zikiwa   na mbegu za kiume
Mshitakiwa  baada ya kufanya kitendo hicho  siku iliyofuata  alimtuma  mama yake mzazi aende  kwa jinana huyo akamwombee samahani  kwa kile alichoeleza kuwa anahofia  kufungwa jela
Baada ya mama mshitakiwa  Wiliamu  George  kumwombea msamaha kwa kijana alilawitiwa  alikubali  kumsamehe  mshitakiwa  kwa kuhofia  kupata aibu
Mshitakiwa baada ya kusamehewa  alianza kumtangaza  kijana huyo  kwa rafiki zake  na  kuwafahamisha kuwa kijana huyo ni shemeji yao  kitendo ambacho kilimkasilisha kijana huyo na kuamua kwenda kituo cha polisi kutoa taarifa ya kulawitiwa  kwake na Mshitakiwa Wiliamu George
Hakimu mkazi mfawidhi Chiganga Ntengwa kabla ya kutowa hukumu hiyo  aliiambia mahakama kuwa  mahakama imemtia hatiani mshitakiwa  Wiliamu  George kwa kosa la kumwingilia  kijana huyo  kinyumbe na maumbile yake hivyo mahakama inatowa na fasi kwa mshitakiwa kama anasababu ya msingi ya kuishawisha mahakama impunguzie  adhabu  aieleza mahakama  hiyo
Katika uetezi wake mshitakiwa aliiomba mahakama imwachie huru kwani  yeye hakutenda kosa hilo na pia umri wake bado ni kijana mdogo na wazazi wake bado wanamtegemea  maombi ambayo yalipingwa vikari na mwendesha mashitaka
Hakimu Chiganga baada ya  kusikiliza  utetezi huo aliiambia mahakama kuwa  mshitakiwa amehukumiwa na  mahakama  baada ya  kupatikana   na hatia ya kumwingilia kinyume na maumbile kijana huyo na  anahukumiwa na adhabu ya kifungu cha sheria  namba  235 sura ya 20 ya mwaka 2009 hivyo Wiliamu George mahakama imehukumu kutumikia jela kuanzia jana kifungo cha miaka 30 jela

No comments:

Post a Comment