Tuesday, December 10, 2013

MKUU WA MKOA WA KATAVI AHIMIZA KILIMO.



DKT RUTENGWE AKIPANDA SHAMBA LA MFANO KWA WAKULIMA MKOANI KATAVI 
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Rajabu Rutengwe akishiriki kupanda mbegu shambani.

Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dkt Rajabu Rutengwe Ametoa changamoto kwa wataalam kuanzisha mashamba darasa katika maeneo yao yatakayotumiwa na wakulima kujifunza kwa vitendo na kuondokana na dhana kulima kwa mazoea kwa kuwa kilimo hicho kimepitwa na wakati na hakina tija.
Dkt Rutengwe alitoa kauli hiyo wakati akishiriki katika shughuli za kilimo kwenye shamba la mfano lililoko kwenye kijiji cha mwenge kwa kuwashirikisha watalaam wa kilimo mkoani humo na wananchi wa kata ya nsimbo kuwaonesha kwa vitendo namna ya kulima kwa kufuata utalaam na maelekezo wanayopewa na maafisa ugani wa kijiji husika kasha akagiza kila Afisa ugani katika eneo lake awe na shamba la kujifunza wakulima ili kile wanachojifunza wakifanyie mazoezi kwenye mashamba yao.
kwa kushirikiana na wananchi wa kijiji cha Mwenge Kata ya Nsimbo wameshiriki kwa vitendo katika kutekeleza azima ya kilimo kwanza kwa vitendo kwa kutoa elimu ya kilimo bora na chenye tija kwa kuwafundisha wakulima kulima kwa kufuata kanuni bora za kilimo kwa kupanda kwa mstari, kwa kutumia mbegu bora na mbolea ya minjingu na Inyala inayotolewa na Kampuni ya Mosanto na mbegu za muda zianzokoma kwa muda mfupi na mrefu kulingana na hali ya hewa ya eneo husika mbali na kulima katika shamba lake hilo ambalo amelitoa kwa wananchi kuwa shamba darasa la kujifunzia pia alishiriki katika zoezi jingine la kupanda shamba la waziri mkuu Mizengo Pinda lililoko kijijini kwake kibaoni ikiwa nalo ni shamba la mfano kwa ajili ya kufundishia wakulima mkoani humo na shamba la kitaifa.
Kwa upande wake Afisa ugani kutoka SAGOT Joanita Elias alieleza kuwa Kampuni ya Mosanto ianyouza mbegu za mahindi aina ya DK na mbolea aina ya Ayara ni kampuni ambayo inatoa mbegu mbole ana mbolea yenye ubora ambayo inasidia kusitawisha mazao kwa muda mfupi na haina madhara.
Akifafanua zaidi alieleza kuwa katika zoezi hilo ambalo lilioneshwa namna ya kupanda kwa msta mahindi ya muda wa kati yanayokoma kwa muda wa siku 120, mahindi ya muda mfupi yanayokoma kwa muda mfupi wa muda siku 90. pia walipandia mbolea ana ya mijingu inayotengenezwa hapa nchini
Chanzo;Full shangwe

No comments:

Post a Comment