Tuesday, December 10, 2013

MADUKA YA DAWA ZA BINADAMU YAFUNGIWA MKOANI KATAVI


MFAMASIA AKIHESABU DAWA DUKANIMoja ya wafamasia kutoka mkoani katavi Hospiltali ya Mkoa wa KATAVI akikagua dawa zilizokutwa ndani ya Famasi ambazo zimendaiwa kuwa Famasi haikufuata sheria kufunguliwa na dawa zilizomo ni nyingi hazilingani na wataalam wanaohudumia Famasi hiyo kulinganana sheria za Famasia.


Baraza la Wafamasia Nchini kwa kushirikiana na wafamasia wa Mkoa wa katavi wamelifungia Duka la dawa muhimu la Semiwe Phamarcy ltd lililoko mjini Mpanda kwa muda usiojulikana kutokana na Phamarcy kukiuka Sheria kanuni na taratibu za uendeshaji wa Phamarcy nchini.
Akizungumzia sababu zilizosababisha kufungiwa kwa Phamarcy hiyo Mfamasia kutoka Baraza la Famasi Taifa Idara ya Afya Bi Suma David Jailo amesema kuwa ni kutokana na Mmiliki wa Phamarcy hiyo kufanya biashara bila kuwa na kibali cha baraza la Famasi ambapo kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.
Sababu nyingine aliitaja kuwa Famasi hiyo ilikuwa haina Mfamasia ambaye ni mtaalam anahusika kusimamamia Famasi kulingana na Sheria za Baraza la Famasi,ambapo mtu anayefungua Famasi kama hiyo inatakiwa ifunguliwe na ipate kibali kutoka Baraza la Famasia lakini yeye hakufanya hivyo wakati akijua taratibu.
Jailo ameleza kuwa kwa sababu hiyo amefanya makosa kwa kwa kukiuka taratibu hvyo kwa makosa hayo yote yaliyokutwa kwenye Famasi hiyo imebidi hatua za awali kuchukuliwa za kuifungia wakati taratibu nyingine za kumfikisha kwenye mamlaka za kisheria zikiendelea.
Akifafanua zaidi Mfamasia huyo kutoka Baraza la Famasi Jailo alieleza kuwa Kwa kuwa sheria wameivunja dawa zote zinakusanywa na kupelekwa kituo cha Mkoa kwa Mkurugenzi ili taratibu za kisheria zifuatwe.
“Duka limekutwa na dawa nyingi ambapo kisheria haziruhusiwi kuwepo katika eneo hili “alisema akaongeza kuwa kwa hili tunatoa ushauri kwa maduka mengine yeyote yahakikishe kuwa yanakuwa na vibali na yafuate sheria zilizowekwa na siyo kufanya kama dukua hili ambalo limekutwa na dawa nyingi amabazo haziruhisiwi kuwepo eneo hili”alisema Suma Jailo.
Akizungumzia Jamii ya wanakatavi waliokuwa wakihudumiwa na Duka hili na wale waliokuwa wakifanya kazi hapo na kupata ujira na hasa watumiaji wad aw alieleza kuwa watu wa maeneo haya watakuwa wameathirika kwa kuwa walikuwa wakitegemea dawa hizo kuwahudumia hata hivyo kwa upande mwingine akaeleza kuwa hatua iliyochukuliwa ni saahihi kwa sababuwatu walikuwa wanapata dawa ambazo siyo sahihi kwa magonjwa waliyokuwa nayo.
Akaongeza kuwa kwa hivyo kwa njia moja au nyingine wameepusha madhara makubwa ambayo yangeweza kuwapata watuamiaji ingewezekana mtu akapata dawa amabayo siyo sahahihi kwa magonjwa aliyo nayo.
Kuhusu wafanyakazi waliokuwa wakifanya kazi katika Famasi hiyo alisema watoa huduma wote waliokuwa ni wahudumu na manesi watupu wauzaji ambao hawana utalaam hakukuwa na Mtaalaam wa kuweza kulingana na ukubwa wa Famasi hiyo anatakiwa awepo mfamasi mwenye sifa sitahiki.
Alisikitishwa kuona kuwa Mmiliki wa Famasi hiyokuwani mfamasia na shreia zote za kuanzisha Famasi anazifahamu na ameishaelezwa na kwa kuwa kilakitu alichofanya ni kosa kulingana na sheria za Baraza la Famasi atapelekwa kwenye Priminari Commity ambapo atachukuliwa hatua za kisheria kulingana na sheria zao.
Kwa upande wake Kaimu Mfamasia wa Mkoa Katavi kutoka ofisi ya Katibu Tawala Mkoa wa Katavi Gabriel Changula ameleza kuwa zoezi hilo litakuwa endelevu na wao wapo kwa ajili ya kusimamia sheria zilizopo na kuwaondolea wasiwasi wananchi kuwa wasiwe na hofu kutokana na dawa walizotumia serikali ipo kwa ajili nya kuweza kusimamia sheria na kutoa maelekezo kwa wananchi wake.
Naye Mfanyakazi katika Duka hilo aliyejitambulisha kwa jina la MWITA Mitiro alioneshwa kushangazwa na maamuzi yaliyochukuliwa kwa kuwa haamini nkama kweli mmiliki wa Duka hilo anaweza kufungua duka bila kuufuata sheria wakati yeye ni Mfamasi na anaelewa taratibu zote za kufuata.
Akaongeza kuwa kufungwa kwa duka hilo kwa njia moja au nyingine kumewathiri watu wengi wanaotegemea huduma ya dawa katika duka hilo kwa kuwa lilikuwa likisaidia watu wengi tena kwa gharama nafuu na pia kwa upande wa watu waliokuwa wanafanya kazi hapo familia zao zitateteleka kwa kuwa kibarua sasa kimeingia mchanga hawana kazi tena kwa muda ambaop watakuwa wamelifunga duka hilo la dawa ni vyema busara ingetumika kuangali apande zote mbili bila kathiri upande mmoja au mwingine na akashauri kama wangeweza kumwita mmliki na kumpatia maelekezo aweze kurekebisha pale palipo na makosa kuliko hatua zilizochukuliwa.
Na Kibada Kibada – Mpanda Katavi  
Chanzo;Full shangwe blog

No comments:

Post a Comment