Thursday, December 19, 2013

AKATWA PANGA KWA UGOMVI WA SHAMBA‏


Na Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
Mtu mmoja  aliyefahamika kwa jina la   Masunga  Nnigo(38)  Mkazi wa Kijiji cha  Tumaini Kata ya Itenka Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi  amejeruhiwa  kwa kukatwa  na mapanga   na watu watatu  kutokana na mgogoro wa kugombea shamba  la Hekta  tatu
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Kamishina Dhahiri Kidavashari  tukio hilo lilitokea hapo  Desemba 15  mwaka huu majira ya  saa moja na nusu asubuhi huko katika kijiji cha  Tumaini
Alisema siku hiyo ya tukio  Masunga alikuwa shambani kwake akilima mazao katika shamba hilo  ndipo  walipotokea watu watatu  wakiwa na panga na kisha walianza kumkata kata  kwenye mkono wa kushoto  na kwenye nyonga  upande wa kushoto huku wakimtaka  asirudie tena kulima kwenye shamba hilo kwani walidai sio mali yake
Masunga baada ya kuona anaendelea kushambuliwa na watu hao alianza kupiga mayowe ya kuomba msaada kwa majirani zake
Alisema majirani baada ya kusikia mayowe ya Masunga walifika katika eneo hilo na kukuta  watuhumiwa hao wakiwa  wamesha tokomea huku   Masunga akiwa anavuja damu kwenye mkono wake  wa kushoto kutokana na  kukatwa katwa vibaya sehemu hiyo ya mkono  
 Majeruhi amelazwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda  ambako anaendelea kupatiwa matibabu huku hari yake  ikiwa  bado  sio nzuri  kutokana na majeraha aliyoyapata
Kamanda Kidavashari  alieleza watu wawili  wanashikiliwa na jeshi la polisi kuhusiana na tukio hilo ambao ni  Ndasa  Wandasa 54 na Mgudi  Ndasa 27  wakazi wa kijiji hicho cha Tumaini ambao wamekuwa na ugomvi wa kugombea shamba na   Masunga
Upelelezi  wa tukio hili unaendelea  na watuhumiwa  watafikishwa Mahakamani  mara baada ya  uchunguzi utakapo kuwa umekamilika  ili waweze kujibu mashitaka yatakayo kuwa yamewakabili

No comments:

Post a Comment