Tuesday, November 12, 2013

INASIKITISHA: AUWAWA KWA KUKATWA KOROMEO AKIWA AMELALA NA MUME WAKE KITANDANI‏.

Na  Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi  

Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Ngoro  Nyengera (60)   mkazi wa Kijiji cha Mirumba  Tarafa ya Usevya Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi ameuwawa kwa kukatwa kolomeo  na kitu chenye ncha kali  nyumbani kwake wakati akiwa amelala kitandani na mume wake.

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari alisema tukio hilo la mauwaji ya mwanamke huyo ya kusikitisha lilitokea hapo juzi majira ya saa saba na nusu usiku nyumbani kwa marehemu ambae alikuwa akiishi na mume wake aitwaye Rina  Kuzenza (70)
Alisema siku ya tukio marehemu alikuwa amelala na mumewekitandani katika nyumba waliokuwa wakiishi pamoja na kijana wao aitwaye  Ndura  Kusenza (20) ambae yeye alikuwa akilala chumba kinachotazamana na chumba cha wazazi wake.

Kamanda Kidavashari alieleza ghafla  watu wawili walivunja mlango wa chumba alichokuwa amelala marehemu na mumewe na kuingia ndani huku wakiwa na tochi kubwa mbili zenye mwanga mkali na kuwaweka chini ya ulinzi wao marehemu na mumewe

Alisema ndipo walipomwamuru mume wa  Marehemu akifunike usoni kwa shuka yake na kisha walimlazimisha alale akiwa amelala kifudifudi

Kidavashari alieleza kuwa baada ya kulazimisha hivyo mumewe  alitekeleza amri hiyo na ndipo watu hao walipoanza kumkata Ngoro Nyengera kolomeo hadi kufariki dunia 

Kamanda Kidavashari alisema siku za nyuma marehemu alikuwa akilalamikiwa  na wanakijiji  wenzake kuwa ni mshilikina  na amekuwa akituhumiwa kuwaloga wanakijiji wenzake hari ambayo ilipelekea marehemu kuchukiwa na kukosa mahusiano mazuri baina yake  na wanakijiji wenzake.

Alisema katika tukio hilo hakuna mtu wala watu waliokamatwa na jeshi la polisi  linaendelea  na upelelezi wa kuwabaini waliohusika katika mauwaji hayo ili kuweza kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria kujibu tuhuma hii ya mauwaji ya kinyama 

IKIWA GAZETI LOLOTE LINATAKA KUTUMIA HABARI HII WASILIANA NASI KWA NAMBA HIZI 0654221465

KATAVI YETU BLOG

No comments:

Post a Comment