Monday, October 21, 2013

WANAOISHI NA VIRUSI VYA UKIMWI WACHAGUA VIONGOZI‏

Na Walter Mguluchuma
Nkasi

Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la watu wanaoishi na virusi vya ukimwi nchini (NACOPHA) Deo Chrispin Mlori ameelezea jinsi vitendo vya unyanyapaa wanavyofanyiwa na baadhi ya watu katika jamii vinavyoathiri ufanisi wao wa utekelezaji wa shughuli za kiuchumi na maendeleo kwa ujumla

Akifungua mkutano wa uchaguzi wa kuunda Baraza la viongozi wa watu wanaoishi na virusi vya ukimwi  liitwalo KONGA uliofanyika juzi mjini Namanyere katika halmshauri ya wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa bwana Mlori alisema waathirika wa ukimwi nao pia wana haki na fursa sawa  ya  kuchangia nguvu zao kwa ajili ya maendeleo ya jamii

Alisema kuanzishwa kwa BARAZA hilo la kitaifa lililoundwa kisheria kwenye mkutano wa watu wanaoishi na virusi vya ukimwi nchini uliofanyika mwishoni mwa mwzi Agost jijini Dae es salaam na baadae kuagizwa kuundwa kwa mabaraza ya wilaya zote nchini ambayo yataitwa KONGA  kuna lengo la  kukabiliana na unyanyapaa na ubaguzi unaotokana na hali ya kuishi na VVU

Bwana Makori aliwaambia wajumbe hao kuwa KONGA zitakazoundwa katika kila halamshauri ya wilaya zitashirikiana na viongozi wa halmashauri husika katika kuweka msukumo katika kuratibu na kusimamia uwezeshaji tiba mafunzo na misada kwa watu wanaoishi VVU na kupinga dhuluma zinazokiuka utu wa mtu  kwa kuunganisha mitandao mbalimbali inayotekeleza program za ukimwi

Alifafanua kuwa Baraza la kitaifa limeunda timu maalumu itakayoratibu uundwaji wa KONGA katika halmashauri zote za mikoa ya Rukwa na Katavi ambapo tayari halmashauri za Manispaa ya Sumbawanga na Sumbawanga mkoani Rukwa na sasa Nkasi na zile za Halmashauri ya Mji wa Mpanda na Halmashauri ya wilaya ya Mpanda mkoani Katavi zimechagua viongozi wake na kubaki halmashauri za Kalambo (Rukwa) na Mlele na Nsimbo (Katavi)

Wajumbe wa uchaguzi huo walielezwa na mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Nkasi Peter Mizinga  ambaye ndiye aliyekuwa msimamizi mkuu kuwa halmashauri ya wilaya ina wajibu wa kushirikiana na viongozi wa KONGA hizi katika kuhakikisha kuwa watu wanaoishi na VVU na wengineo wasiokuwa na virusi kuzuia kuenea kwa maambukizo mapya

Alisema halamshauri ya wilaya ya Nkasi itaanda utaratibu utakawashirikisha viongozi wa baraz a la wilaya katika kutoa mafunzo kwa njia ya mikutano semina na makongamano yatakayokuwa yanaendeshwa katika maeneo mbalimbali kuanzia ngazi za vijiji kata hadi Tarafa na hata kwenye vikao vya baraza la madiwani wa halmashauri hiyo

Mratibu wa ukimwi katika halmashauri hiyo Filbert Msapila aliwahahakikishia wajumbe wa kikao hicho na viongozi wake kuwa ushirikiano wao na halmashauri utawezesha kujenga uwezo wa Taasisi za watu wanaoishi na VVU ili waweze kumsaidia  mtu mmoja mmoja na au familia zao kupitia program zao

Bi Edinatha Matandiko aliyechaguliwa kwa kura zote 21 za wajumbe kuongoza baraza la viongozi 10 wa KONGA ya wilaya ya Nkasi alisisitiza umuhimu wa mitandao yote inayojihusisha na ukimwi chini ya BARAZA la kitaifa na KONGA za wilaya kusimamia kulinda na kuteteta haki za watu wanaoishi na virusi vya ukimwi katika jamii na kuwa na mikakati endelevu ya kukabiliana na maambukizo mapya

No comments:

Post a Comment