Wednesday, May 29, 2013

POLISI WAKAMATA LITA 70 ZA GONGO‏

Walter Mguluchuma-Katavi yetu Blog

Jeshi la polisi mkoani katavi limewakamata watu wawili katika matukio mawili tofauti wakiwa na pombe haramu ya gongo lita 70
Kaimu kamanda wa polisi wa mkoa wa Katavi Emmanuel Nlay aliwataja waliokamatwa kuwa ni Marietha Ngalawa (59) mkazi wa kijiji cha Tukoma na January Katalambula (33) mkazi wa kijiji cha Mtisi wote wanatoka wilaya ya Mlele
Katika tukio la kwanza Marietha alikamatwa na lita 10 za pombe haramu ya gongo zikiwa zimehifadhiwa nyumbani kwakwe
Kaimu kamanda Nlay alisema tukio hilo limetokea hapo mei 21 mwaka huu majira ya saa 6 mchana.
Tukio la pili lilitokea hapo mei 25 majira ya saa 12 jioni ambapo January Katambala alikamatwa na lita 60za pombe haramu ya gongo zikiwa zikiwa ndani ya nyumba yake.
Alieleza watuhumiwa hao walikamatwa kufuatia taarifa zilizolifikia jeshi la polisi kuwa watu hao wanajishughulisha na biashara haramu ya pombe aina ya gongo
Upelelezi wa matukio haya yote mawili umekamilika na watuhumiwa wanatarajiwa kufikishwa mahakamanai kujibu mashitaka

No comments:

Post a Comment