Tuesday, April 5, 2016

WAZIRI ATAKA WAKANDARASI KUFANYA KAZI KWA KUZINGATIA VIWANGO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
   Katavi
Waziri wa  Ujenzi  Uchukuzi na Mawasilano Pro Makame    Mbarawa  amewaagiza wakandasi  wote  hapa  Nchini  waakikishe wanafanya  kazi zao kwa wakati  na kwakuzingatia  viwango  vinavyo  takiwa .
Agizo  hilo  alilitowa  hapo juzi wakati alipokuwa  akizungumza  na  viongozi wa  Mkoa  wa  Katavi  kwenye  ofisi ya Mkuu wa  Mkoa  wa  Katavi  wakati wa  ziara  yake  ya  siku  mbili  Mkoani   hapa  .
Alisema  lengo la  Wizara  yake  ni kuwajengea  Watanzania  miundo  mbinu ya kisasa  ya  kisasa hivyo wizara  haiku  tayari  kuona  mkandarasi   anashindwa kufanya  kazi kwa  wakati  na kwa kutozingatia viwango .
Waziri  Mbarawa  aliwaka  wafanyakazi wa  wakala za  barabara  hapa  nchini  Tanroods  wafanye  kazi   kwa  uadilifu  mkubwa  ili kuhakikisha  watanzania  wanapata  huduma   bora  na kasi  inayotakiwa.
 Alisema  Serikali  imeisha  anza kuwalipa  fedha wakandasi  hivyo miradi  ambayo ya ujenzi wa  barabara  iliyokuwa imesimama  itaendela  kama  kawaida na itakamilika   kama  ilivyo  kuwa  imepangwa .
Kuhusu  mawasiliano  alisema  Serikali  itahakikisha  maeneo  yote ya  pembezoni  na  mikani  kuna  kuwa  na  mawasiliano ya uhakika  ukiwemo  na  Mkoa  wa Katavi  ambao  baadhi ya  maeneo  mawasiliano ya  simu  hayapatikani .
Pro  Mbarawa  alieleza  kuwa  serikali  imepanga kununua  ndege mbili kwa ajiri ya  shirika  la  ATC  na  wamepanga  dende  moja  itakuwa  inafanya  safari  zake  katika  Mji wa  Mpanda  Mkoani  Katavi  na Mikoa  ya  Kigoma  na  Dares salam  kwani  mikoa  ya  Katavi na  Kigoma  bado  haina  ushindani  wa  wa  makampuni   ya  ndege .
Alisema  uwanja wa  ndege wa  Mpanda  uliojengwa kwa kiwango cha  rami  1.8 unasifa  zote za kutuwa kwa ndege  ndogo  hivyo wizara  yake itaondoa  changamoto  inayoukabili  uwanja  ya ukosefu wa gari la  zima  moto  hivyo  gari  hilo litapatikana  hivi  karibuni .
Alizungumzia  reli ya  Mpanda  alisema   usafiri wa  treni  kutoka  Mpanda  hadi  Tabora  hauta  simama kwani  Wizara  imejipanga na kuhakikisha  huduma hiyo  inapatikana wakati  wote na pia  Serikali  inampango wa  kujenga  reli kutoka  Mpanda  hadi  Karema  itakayokuwa inatumika kusafirishia  mizogo  hadi  kwenye  bandari inayojengwa katika  Ziwa  Tanganyika  huko   Karema na  mizigo hiyo kuelekea  Nchi  ya  Kongo.
Awali Mkuu wa  Mkoa  wa  Katavi  Major  Jenelali  mstaafu  Raphael   Luhuga alimweleza  Waziri  huyo  kuwa  Mkoa  huo  unachangamoto kubwa ya   barabara kuwa  nyingi  za  udongo  na  changarawe kwani  hadi  sasa  unabarabara ya  rami kiasi cha  kilometa  34 tuu  hari  ambayoimekuwa  ikisababisha watu washindwe kusafirisha   mazao yao .
Alisema  kutokana  na  barabara  hizo kuwa za  udongo  na  changarawe  zimekuwa zikiharibika  sana  hasa  wakati wa  masika  na pia  wanakabiriwa  na  changamoto ya  uwanja wa ndege kukosa  kituo cha kuongezea  mafuta ya  ndege   katika   uwanja  wa  ndege wa  Mpanda na ndio inaweza ikawa  sababu ya MKoa  huo  kukosa  usafiri wa  ndege.

No comments:

Post a Comment