Friday, March 18, 2016

ZAIDI YA WATU 9,000 WAPIMA VVU WATU 334 WALIGUNDULIKA KUWA NA VVU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na    Walter  Mguluchuma
    Katavi
 Jumla ya watu  ya watu 9,000 wamepima  VVU    Wilayani Mpanda  Mkoa wa Katavi katika kipindi cha  mwezi  Oktoba hadi Desemba  2015 na wateja zaidi ya  300 waligundulika kua na maambukizi ya VVU  ikiwa ni sawa na asilimia 3.5
Hayo yalisemwa hapo jana na  mratibu wa kuthibiti ukimwi wa Wilaya ya Mpanda Dk  Benald Kamande wakati akisoma taarifa ya utekelezaji  huduma za  ukimwi  katika  Wilaya ya Mpanda  kwa kipindi  cha Oktoba   hadi Desemba 2015 mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Mpanda  Paza Mwamlima katika ofisi ya mganga mkuu wa Wilaya ya Mpanda.

 Alisema  idadi ya wateja  waliopimwa   VVU katika Wilaya hiyo na kupatiwa majibu yao ni 9,487 na idadi ya wateja waliogunduliwa kua na maambukizi ya VVU ni  334 sawa na asilimia 3.5
Dk vituoKamande alieleza  katika kipindi hicho  wateja  wapya  walioandikishwa  katika vituo tiba na  kupatiwa mafunzo  ni 235. Na wateja wapya  walionzishiwa dawa ARVs kwa kipindi hichi  ni 187.
Mpaka sasa  idadi ya  wateja wanao   dawa  za ARVs hadi kufikia  Desemba mwaka jana  katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ni wateja 2186.
 Alisema kumekuwapo na changamoto mbalimbali  katika utekelezaji  wa huduma za ukimwi  Wilayani Mpanda  baadhi ya changamoto hizo ni utoro wa watumiaji wa dawa ARVs unasababishwa na umbali wa vituo vya kutolea huduma na wateja wengine wamekuwa wakitumia majina bandia.
Changamoto  nyingine ni  ukosefu wa usafiri wa gari la kutowa huduma za CTC   na ukosefu wa umeme kwenye vituo na motisha mdogo kwa watowa huduma.
Nae mkuu wa kitengo cha CTC katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Dr Benson Luhende katika kipindi hicho cha mizi mitatu ya oktoba hadi desemba mwaka jana  wateja 13 walifariki Dunia.
Alisema toka kituo  kianze kutowa huduma  wateja walioandikishwa  ni  5521 kati yao wanaume  ni 2348 na wanawake 3,173 na waliko kwenye ARVs ni wanaume  712 na wanawake 883.
Kwa upande wake mkuu wa Wilaya ya Mpanda Paza Mwamlima  alisema kazi wanayofanya watumishi wa afya ni ngumu hivyo alimtaka mkurugenzi  wa Halmashauri ya Wilaya hiyo na Mganga mkuu kuangalia namna ya kuwapatia motisha watumishi hao ili waendelee kuwa na moyo zaidi wa kufanya kazi .
 Alisema motisha sio lazima iwe ni kuwapatia fedha tuu mnaweza kufanya utaratibu wa kuwapeleka watumisha hao kwenda kutembelea mbuga ya hifadhi ya Katavi au kuwapeleka kwenda kuliona ziwa Tanganyika.

No comments:

Post a Comment