Monday, March 14, 2016

HATARI: MUUGUZI ANUSURIKA KIPIGO ,APELEKEWA MWILI WA MAREHEMU NYUMBANI KWAKE BAADA YA NDUGU KUDAI MUUGUZI HUYO AMESABABISHA KIFO CHA MGONJWA HUYO.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Na  Walter  Mguluchuma
Katavi yetu blog
Muuguzi wa Zahanati ya Kapalamsenga Wilayani Mpanda  Rehema Munga amenusurika kipigo na kupelekewa mwili wa marehemu nyumbani  kwake  baada ya wananchi wa Kijiji hicho kumtuhumu kuwa amesababisha kifo cha mgonjwa baada ya kukataa kumpatia huduma za matibabu  wakati wa usiku.
Tukio hilo la muuguzi huo kutaka kupigwa na kupelekewa mwili wa marehemu lilitokea hapo juzi majira ya saa kumi usiku katika kijiji cha Kapalamsenga Tarafa ya Karema  na kulazika  nyumba ya mganga huyo kuwa chini ya ulinzi wa askari wa jeshi la Wananchi wa Tanzani wa Kikosi cha Ikola.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda Hamad Mapengo aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa  wananchi hao walipandwa na hasira baada ya kumtuhumu mganga huyo kuwa amesababisha kifo cha Bibiana Karangi 49 kwa kuchelewa kumpatia huduma za matibabu kwa wakati.
 Alisema siku hiyo ya tukio majira ya saa saba  usiku marehemu huyo alifikishwa katika zahanati hiyo na walipohitaji huduma ya matibabu kwa kumwamsha mganga huyo aliyekuwa nyumbani kwake kwenye eneo la zahanati hiyo alikataa  kuamka  na aliwataka wampeleke mgonjwa huyo  katika kituo cha afya cha Karema .
Mwenyekiti huyo alieleza  mgonjwa huyo alipelekwa hadi kwenye kituo cha afya Karema na kugundulika kuwa anatatizo la upungufu wa damu hivyo anatakiwa apelekwe katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda na wakati akiwa hapo alifariki baada ya muda si mrefu .
Baaada ya Bibiana kufariki Dunia baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Kapalamsenga  walipata taarifa ya  kifo hicho na ndipo walipoamua kujikusanya kwa lengo la kwenda kituo cha afya cha Karema ili wakachukue mwili wa marehemu na  kuupeleka  chumbani kwa mganga wa zahanati  hiyo kwa kile walichodai kuwa ndiye aliyesababisha kifo hicho kwa kutompatia huduma na mapema .
Viongozi wa Kata hiyo walipata taarifa hizo hari ambayo iliwalazimu waombe msaada kwa askari wa Jeshi la wananchi wa kituo cha ikola ambao walifika kwenye eneo hilo na  kuizingira  nyumba ya mganga wa zahanati hari ambayo  iliwalazimu wananchi hao kuanza kutawanyika kwenye eneo hilo .
Hamad Mapengo alieleza  kuwa ilimlazimu yeye na kaimu mganga mkuu wa Wilaya ya Mpanda Dk Naibu Mkongwa wachukue uamuzi wa kwenda  kumchukua  mganga huyo na  kumpeleka Mpanda Mjini kwa kuhofia hari ya usalama wake.
Afisa Tarafa wa Karema  Zawadi Mirambo jana alilazimika kwenda kijijini hapo na kufanya kikao na wananchi  hata hivyo kwenye kikao hicho maoni ya wananchi hao yalitofautiana  na wauguzi wa zahanati hiyo ambapo wauguzi walidai kuwa marehemu huyo alikuwa meisha ugua muda mrefu na alikuwa ameisha ambiwa akatibiwe kwenye kituo cha afya cha Karema toka muda mrefu .
Wananchi wao walidai kuwa  imekuwa ni kitendo cha mara kwa mara  mganga huyo kukataa kutowa huduma kwa wagonjwa nyakati za usiku kutokana na hari yake ya ujauzito.
Kabla ya kikao hicho cha afisa Tarafa na wananchi   Mtendaji wa Kata hiyo aliokota barua  ambayo ilandikwa na watu wasiojulikana ikiwa inaeleleza kuwa mganga huyo hawataki kumwona tena akitowa huduma kwenye zahati hiyo na wala asionekane tena kijijini hapo .
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda ameunda tume ya kufatila tatizo hilo ilikuweza kupata ukweli kuhusiana na tuhuma za wananchi .

No comments:

Post a Comment