Wednesday, February 3, 2016

HATARI: MWANAMKE ACHOMWAKISU NA MPENZI WAKE WAKATI WAKIWA WAMELALA GESTI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



Na  Walter Mguluchuma
 Katavi yetu Blog
Mwanamke mmoja  aliyejulikana kwa jina la  Zuhura Salumu 34 Mkazi wa Mtaa wa Majengo Wilaya ya Mpanda  amejeruhiwa kwa kuchomwa na kisu  katika titi lake la kulia wakati akiwa wakiwa wamelala na mpenzi wake kwenye nyumba ya kulala wageni inaitwa Maridadi iliyoko  katika Mtaa wa Majengo B mjini Mpanda.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari alisema mbele ya waandishi wa Habari kuwa tukio  lilitokea hapo juzi katika nyumba ya kulala wageni inayoitwa Maridadi katika Mtaa wa Majengo.

Alisema siku hiyo ya tukio Zuhura  alikuwa amelala kwenye nyumba hiyo ya kulala wageni huku akiwa amelala  na mpenzi wake anaitwa  Iddy  Salehe.

Kamanda Kidavashari wakati wakiwa wamelala mtuhumiwa  Iddy  Salehe  aliamka  na kumvizia  Zuhura wakati akiwa usingizini na kumchoma kisu kwenye titi lale la kulia  na kumjeruhi vibaya.

 Alieleza  kitendo hicho kilimfanya Zuhura apige mayowe ya kuomba msaada na aliweza kusaidiwa na walinzi wa nyumba ya kulala wageni hiyo na ndipo walipofanikiwa kumkamata mtuhumiwa na waliweza kutowa taarifa polisi ambao walifika kwenye eneo hilo baada ya muda mfupi.

Kidavashari alisema chanzo cha tukio hilo bado  akijajulikana  mpaka sasa  kilichopelekea mtuhumiwa  kufanya kitendo hicho kisicho   cha  kawaida.

Mtuhumiwa  Iddy Salehe  bado anashikiliwa na jeshi la Polisi  kwa mahojiano zaidi na anatarajiwa kufikishwa Mahakamani  kujibu tuhuma inayomkabili.

No comments:

Post a Comment