Saturday, December 19, 2015

WAWILI JELA MIAKA 42 KWA KOSA LA KUKAMATWA NA MENO YA TEMBO YA MILIONI 60

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
Mahakama ya Wilaya ya Mpanda Imewahukumu watu wawili  kifungo cha miaka 42 jela  baada ya kupatikana na hatia ya kukamatwa na meno ya Tembo manne   yenye thamani ya shilingi milioni sitini
Hukumu hiyo ilitolewa hapo jana na Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda  Odira  Amwol baada ya mahakama kulidhika na ushahidi uliotolewa Mahakama na upande wa mashitaka.  
 Watuhumiwa hao waliohukumiwa kifungo hicho cha kwanda  jela ni  Justine Bruno(50)  Mkazi wa Kijiji cha Usevya  na  Filiberti Leo(35) Mkazi wa Kijiji cha Ikuba    wote wawili wakazi wa Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi.
Awali katika kesi hiyo  mwendesha  mashitaka mwanasheria wa Serikali  Jamila   Mziray aliiambia Mahakama kuwa watuhumiwa hao wote  wawili walikamatwa na meno ya tembo hapo Novemba 17 mwaka huu majira ya usiku katika kijiji cha Ikuba Wilayani Mlele.
Siku  hiyo ya tukio watuhumiwa hao walikamatwa na Askari  wa jeshi la Polisi Mkoa wa Katavi kwa kushirikiana na Askari wa TANAPA wa Mbuga ya Katavi huku wakiwa wamepakia kwenye pikipiki meno ya Tembo manne yenye  uzito wa kilogramu 47.6 yenye thamani ya shilingi milioni sitini.
Upande wa mashitaka  katika  kesi hiyo ulikuwa na mashahidi watano na washitakiwa  walikuwa hawana shahidi yoyote hivyo walijitetea wenyewe .
Hakimu   Amwol  kabla ya kusoma hukumu hiyo aliiambia Mahakama kuwa kutokana na mwenendo mzima wa kesi hiyo mahakama pasipo shaka yoyote imewatia washitakiwa hatiani  hivyo  kabla ya kutolewa kwa hukumu  anawapa nafasi washitakiwa  kama wanasababu yoyote ya msingi ya kuishawishi mahakama iwapunguzie adhabu  anatowa nafasi kwa washitakiwa kujitetea.
 Washitakiwa  katika utetezi wao waliiomba Mahakama iwapunguzie adhabu kwa kuwa wanawazazi na watoto ambao wanaowategemea .
Mwanasheria wa Serikali alipinga vikali maombi hayo na kuiomba mahakama itowe adhabu kali kwa washitakiwa kwani  tatizo la ujangili katika Mkoa wa Katavi limekuwa likiongezeka siku hadi siku hivyo wapewe adhabu ambayo itakuwafundisho na kwa watu wengine wenye tabia kama hizo.
Akisomo  hukumu hiyo Hakimu  Amwol aliiambia Mahakama kuwa  washitakiwa wamepatikana na kosa la  kuvunja sheria  ya  uwifadhi wa  wanyama  kifungu  86(1) 2b na c na kifungu  cha sheria  cha makosa ya  kupanga  na  kuhujumu uchumi  No  57  (1)(60)  sura ya 200 marejeo ya 2002.
Hivyo kutokana na kupatikana na kosa hilo  Mahakama  imewahukumu  Justine Bruno  na Filiberti Leo kutumikia  kifungo cha miaka 21  jela kwa kila mmoja .

No comments:

Post a Comment