Na Walter Mguluchuma
Katavi yetu Blog
Mwili wa Mfugaji
wa mifugo Moshi Salehe (17) Mkazi wa Kijiji cha Kamsisi Wilaya ya Mlele
Mkoani hapa umeshindwa kuzikwa na ndugu zake na bado unahifadhiw katika
chumba cha kuhifadhi maiti cha Hospitali ya Wilaya ya Mpanda kwa muda wa siku
tatu sasa baada ya baba mzazi wa
marehemu na ndugu zake kukataa kuuzika kwa kila wanachodai mpaka hapo watakapo kuwa wamechukuliwa hatua
Askari wa wanyama pori wa TANAPA wanaosadikiwa kumuuwa kwa kupiga risasi
Kwa mujibu wa baba
mazazi wa marehemu Samweli Daki
aliwaambia jana waandishi wa habari kwenye jengo la
kuhifadhia maiti la hospitali ya
Wilaya ya Mpanda kuwa marehemu mtoto wake alifariki Desemba 6 majira ya saa kumi jioni katika
eneo la Kanono wilayani Mlele
Alisema kuwa siku hiyo ya tukio yeye akiwa na
marehemu na watoto wake wengine watano walikuwa wakiswaga Ng’ombe zao kutoka
Kata ya Mpanda ndogo Wilaya ya Mpanda
wakiwa wanaelekea Kijiji cha Kamsisi
Wilayani Mlele walikokuwa
wanahamishia makao yao
Alieleza ndipo walipofika kwenye eneo hilo
ambapo marehemu alikuwa akiswaga ng’ombe
hizo kwenye kichaka
alipokutana na askari hao wa TANAPA wa hifadhi ya Katavi waliokuwa dolia kwenye
gari lao na walianza kuwafyatulia risasi na ndipo risasi moja ilipo mpiga
marehemu kwenye paja lake huku wale alikuwa nao msafara mmoja waliamua wao kutokomea
Samweli
alieleza baada ya kuwa wamempiga risasi hiyo askari hao waliondoka na
kumwasha porini bila kumpatia msaada
wowote ule na waliondoka na gari lao kuelekea njia ya kwenda Mpanda Mjini
Baada ya
muda walikwenda kwenye eneo hilo na
kumchukua marehemu na kumsogeza
barabarani kwa ajiri ya kupata msaada wa kummpeleka hospitali hata hivyo
alifariki baada ya muda kutokana
na kuwa amevuja damu nyingi
Kwa upande wake Mwenyekiti wa wafugaji wa Wilaya
ya Mlele Zenge Luhanga
alieleza kuwa anaungana na ndugu
wa marehemu kuwaunga mkono kwa uamuzi
wao wa kutokubali kuzika mwili wa marehemu mpaka wahusika wa tukio watakapo
kuwa wamechukuliwa hatua
Alisema
wako tayari kushirikiana na ndugu wa marehemu hata kama itakuwa ni mwezi
mzima huhakikisha mwili wa marehemu
auzikwi mpaka watuhumiwa watakapo kuwa wamekamatwa
Kaimu Kamanda wa
Polisi wa Mkoa wa Katavi Rashid Mohamed
alikiri kutokea kwa kifo cha marehemu huyo ambae ni mfugaji wa mifugo
Alisema marehemu huyo aliuwawa kwa kupigwa risasi na
Askari wa wanyama pori waliokuwa wakifanya doria
Kaimu Kamanda Rashid Mohamed alisema jeshi la polisi Mkoa wa Katavi
limeisha chukua hatua kwa kuwakamata na
linawahoji Askari wa Wanyama Pori wa TANAPA walitajwa kuhusika katika tukio
hilo
No comments:
Post a Comment