Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi yetu Blog
Chama cha
Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
Mkoa wa Katavi kimemuengua mgombea wake
wa kugombea Ubunge wa Jimbo la Kavuu Mkoa wa Katavi Amos Mayala
ambae alikuwa amechukua fomu kwa msimamizi wa uchaguzi wa
Jimbo la Kavuu kwa kile kinachodaiwa kuwa
uteuzi wake uliofanywa na ngazi ya Wilaya ni kinyume na taratibu za
Chama hicho
Katibu wa
CHADEMA wa Mkoa wa Katavi Almasi
Ntije alisema kuwa
uamuzi wa kumwengua Amos
Mayala ulifanywa jana
na viongozi wa chama hicho wa Mkoa wa Katavi
baada ya kubaini kuwa uteuzi wake ulifanywa kimakosa na viongozi wa Chama
hicho wa Wilaya ya Mlele
Alisema
chama hicho kimemteuwa
Laulenti Mangweshi kuwa ndio mgombea wa
Ubunge kupitia umoja wa UKAWA
kama ambavyo kamati kuu ya
CHADEMA ilivyokuwa imemteuwa Mangweshi
kuwa ndio mgombea wa ubunge wa Jimbo hilo (CHADEMA)
Alifafanua kuwa
viongozi wa CHADEMA wa Wilaya ya
Mlele hawakuwa na mamlaka ya
kumteuwa Mayala kuwa ndio mgombea wa Jimbo hilo
kwani taratibu za chama
hicho uteuzi wa wagombea
ubunge hufanywa na kamati kuu ya
Chama hicho
Ntije alisema
baada ya kuwa wamegundua uteuzi huo ulikuwa na kasoro walimwandikia barua
msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Kavuu wa kuliondoa jina
na Amos Mayala
na badala yake mgombea halali wa
chama hicho ni Mangweshi
Alisema
ingawa hapo awali baada ya
Amos Mayala kuandikiwa
barua na viongozi wa chama hicho wa Wilaya ya Mlele ya kumtambulisha kwa
msimamizi wa uchaguzi kuwa ndio mgombea wao msimamizi wa uchaguzi alimkabidhi
fomu za kugombea ubunge wa Jimbo hilo na kisha alikwenda
mahakamani na kuapa kiapo hivyo
Chama hicho kilifanikiwa kumuwahi
kabla haja rudisha fomu hizo
Katibu huyo wa
Chadema wa Mkoa wa Katavi
alieleza kuwa jana walifanikiwa kukamilisha taratibu
za kuchukua fomu za mgombea wao wa
Ubunge wa Jimbo la Kavuu Laulenti Mangweshi na mara baada ya kukamilisha
taratibu hizo fomu hizo zilikabidhiwa na
kupokelewa na msimamizi wa uchaguzi wa jimbo la Katavi Godwin Bene
Katika kura za
maoni za chama hicho Mangweshi alikuwa
ni mshindi wa kwanza na Mayala alikuwa ni mshindi wa pili na uteuzi uliofanywa hivi karibu na kamati kuu ya
Chadema ulimteuwa Laulenti Mangweshi kuwa ndio mgombea wa jimbo la Kavuu
No comments:
Post a Comment