Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Walter
Mguluchuma
Katavi
Halmashauri
ya Mji wa Mpanda
Mkoa wa Katavi
ambayo imepandishwa hivi
karibuni kuwa Halmashauri ya Manispaa hadi
kufukia june 30 mwaka huu ilikuwa
imepokea kiasi cha
zaidi ya shilingi milioni
437 kwa ajiri ya matengenezo ya barabara
zake kwa mwaka wa fedha wa 2014
na 2015
Hayo
yalisemwa hapo juzi na Mwenyekiti wa
Halmashauri ya Mji wa
Mpanda Enock Gwambasa
wakati wa kikao cha mwisho cha
baraza la Madiwani
wa Halmashauri hiyo
kilichofanyika katika ukumbi waHalmashauri ya Manispaa ya
Mpanda
Alisema
katika mwaka wa
fedha wa 2014 na 2015
Halmashauri hiyo ilitenga
kiasi cha shilingi
Bilioni moja
milioni mia moja
ishirini na moja na miatano
elfu kwa ajiri ya matengenezo ya
aina mbalimbali ya
barabara kutoka mfuko wa
barabara (ROAD FUND )
Alifafanua
hadi kufikia june 30
mwaka huu Halmashauri yake ilikuwa imepokea kutoka
Serikalini kiasi cha
jumla ya Tsh 437,565,635.16 ambazo ni sawa na asilimia
39 ya bajeti yake yote ya matengenezo ya barabara kwa
mwaka fedha wa 2014 na 2015
Alisema
hadi kufukia june
30 mwaka huu Halmashauri ya ilikuwa
imeingia mikataba saba
ya matengenezo ya Barabara
yenye gharama ya Tsh 632,924,000 kwa ajiri ya matengenezo
ya barabara za mji wa Mpanda
Gwambasa alielez
a katika utekelezaji wa kazi za barabara kumekuwepo na changamoto mbalimbali
ambazo zimekuwa zikijitokeza
Alizitaja
baadhi ya changamoto hizo kuwa ni
makandarasi wengi walioko
Mkoa wa Katavi hawana mitambo
yao kwa matengenezo ya
barabara na badala yake hutegemea mitambo
ya kukodi kitu ambacho hufanya kuchelewa kuanza utekelezaji w kutengeneza barabara
Changamoto
nyingine aliitaja kuwa ni fedha
zinazotengwa kwa mwaka kwa ajiri ya matengenezo ya barabara ni kidogo hivyo hazitoshelezi mahitaji halisi
Pia makandarasi wengi hawana
mitaji ya kutosha hivyo huwafanya
washindwe kuanza kazi kwa wakati unaokuwa umepangwa
No comments:
Post a Comment