Sunday, March 15, 2015

HALMASHAURI YA MJI WA MPANDA KUTUMIA ZAIDI YA BILIONI 18 KWA MWAKA WA FEDHA WA 2015 NA 2016

 
Na  Walter  Mguluchuma
Katavi
 Halmashauri ya Mji wa Mpanda  Mkoa wa Katavi  kwa mwaka wa fedha wa 2015 na 2016 inatarajia  kutumia  na kukusanya  Tsh 18,696,186,334.00 kutoka  katika vyanzo  vyanzo mbalimbali  vya mapato
 Hayo yalielezwa hivi karibuni na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda Selemani Lukanga wakati wa  kikao cha sita  cha kamati ya  ushauri ya  Mkoa wa wa Katavi kilichofanyika  katika ukumbi wa Idara ya Maji  mjini  hapa
Akisema kati ya fedha hizo   Ruzuku  kutoka Serikali kuu  itakuwa ni kiasi cha Tsh 16,507,934,362.00 ambapo  mishahara itakuwa ni kiasi cha  shilingi Biloni 9.3 Ruzuku ya matumizi ya kawaida itakuwa ni Tsh 1,167,392,200.00
Fidia ya mapato yaliyofutwa  Tsh 233,328,500.00 na ruzuku ya miradi ya maendeleo  katika Halmashauri  hiyo  ni kiasi cha  Tsh 5,746,673,662.00
 Lukanga alifafanua kuwa mapato ya ndani ambayo yatatokana na   vyanzo vya mapato  vilivyoko katika Halmashauri ya Mji wa Mpanda wanatarajia kukusanya Tsh 1,147,482,972.00
 Alisema miradi ya maendeleo  kwa mwaka wa fedha  wa 2015 na 2016    imegawanywa katika sehemu mbili  kuu ambazo ni miradi  mipya   na miradi viforo
Alieleza  pamoja na kuandaa  bajeti hiyo   kwa kufuata  vipaumbele   vilivyopo  maksio  yameathirika  kutokana  na   viwango  vidogo  vilivyowekwa  na TAMISEMI  na HAZINA  hivyo  hali  hii  imefanya   mambo  muhimu  zaidi  kutoweza  kutengewa  fedha au  kutengewa fedha kidogo  sana  hivyo kutoleta  matokeo stahili
Alisema kutokana na hari hiyo  Halmashauri  imewasilisha   maombi maalumu  nje ya ukomo  wa Bajeti  yenye jumla ya Tsh 2,988,500,000.00 hivyo kufanya  jumla ya Tsh   21,684,686,334.00  zinazoombwa kwa  mwaka wafedha   ujao  yaani Tsh 18,684,686,334.00 bajeti ya kawaida  na  Tsh  2,988,500,000.00 maombi maalumu



Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

No comments:

Post a Comment