Na Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
Mahakama ya Wilaya ya Mpanda
Mkoa wa Katavi imemuhukumu Philipo Emanuel (35)Mkazi wa Mtaa wa Mpanda
Hotel mjini Mpanda kifungo cha miaka 30 jela baada ya kupatikana
na kosa la kumbaka shemeji yake msichana (13) mdogo wa mke wake mdogo
Hukumu hiyo imetolewa hapo juzi na
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama ya Wilaya ya Mpanda Chiganga Ntengwa
baada ya mahakama kulidhika na ushahidi
uliotolewa mahakamani hapo na pambe zote
mbili za upande wa mashitaka na utetezi
Mshitakiwa alidaiwa kutenda kosa hilo la kumbaka mdgo wa
mke wake hapo Septemba 24 mwaka jana
majira ya saa moja na nusu usiku huko katika eneo la mtaa wa Nsemlwa mjini Mpanda
Awali katika kesi
hiyo mwendesha mashitaka Godfrey
Ruzabila aliiambia mahakama kuwa siku hiyo ya tukio msichana huyo
aliyebakwa alikuwa ametumwa dukani na dada yake kwenda
kununua mafuta ya kupikia mlo wa jioni
Alieleza wakati msichana huyo akiwa anaelekea dukani ndipo alikutana na mshitakiwa ambae alimwita msichana
huyo na kisha alimwomba amsindikize dukani alikokuwa anakwenda kununua mafuta ya kula aliyokuwa ametumwa na dada yake
Mwendesha
mashitaka alidai baada ya kuwa wamefika
dukani msichana huyo alinunua
mafuta na kisha mshitakiwa alimweleza shemeji yake kuwa
anataka kumnunulia zawadi dukani
hapo hivyo achague kitu gani anachokihitaji ndipo msichana huyo
alipomweleza shemeji yake kuwa yeye anahitaji Biscut na Pipibomu
Mshitakiwa baada
ya kumnunulia shemeji yake zawadi hizo alimtaka amsindikize alikokuwa
akienda ombi ambalo msichana huyo alilikubali kwani
hakuwa na mashaka yoyote ya kusindikizwa
na shemeji yake
Mwendesha
mashitaka alieleza wakati wakiwa njiani
mshitakiwa Philipo Emanuel alimwingiza
msichana huyo kwenye pagara na kisha
alipiga ngwala na kuanza kumbaka huku msichana akijaribu kupiga mayowe ya
kuomba msaada lakini alishindwa kutokana na mshitakiwa muda wote kuwa amembana mdomo
Alieleza baada ya kuwa
amemaliza kumfanyia unyama huo
alipatia mtoto huyo shilingi elfu moja
kama malipo yake na shilingi elfu tano alimpatia iliamfikishie dada
yake na alimkaza asimwombie mtu yoyote yule kuwa amefanyiwa kitendo
hicho na mshitakiwa
Ruzabila
alisema baada ya msichana kufika
nyumbani kwao dada yake alimuuliza
kwanini amechelewa kurudi ndipo
binti huyo alimweleza dada yake njisi ambavyo shemeji yake alivyomfanyia hari
ambayo ilmshitua dada yake na kumfanyaachukue
uamuzi wa kumvua nguo na kumkagua katika sehemu zake za siri na kukuta anatokwa na damu hari ambayo
ilimfanya ashituke na kupelekea kuamua
kutoa taarifa kwa wapangaji wenzake
Alieleza dada wa
binti na majirani walimtaka msichana
huyo awapeleke kwenye eneo alilofanyiwa unyama huo na walipofika kwenye eneo la
tukio waliingia ndani ya pagala na kukuta Paketi ya Biscuti aliyokuwa
amenunuliwa na shemeji yake huku pembeni
kukiwa na mafuta ya kula yaliyomwagika na ndipo walipo amua kwenda kituo cha
polisi cha mpanda na kutoa taarifa
Katika kesi
hiyo upande wa mashitaka ulikuwa na
mashahidi wanne akiwemo Daktari ambae
alithibitishakuwa msichana huyo alifanyiwa kitendo cha ubakwaji baada ya
kufanyiwa uchunguzi wa kidakitari
na kukutwa na mbegu za kiume na
upande wa utetezi ulikuwa na mashahidi wanne
Hakimu mkazi Chiganga Ntengwa baada ya kusikiliza mwenendo mzima wa
kesi aliiambia mahakama kuwa mshitakiwa
Philipo Emanuel amepatikana na
hatia ya kosa la kifungu namba 130 (1)
(2) hivyo mahakama inampa nafasi
mshitakiwa kabla ya kutolea kwa adhabu kama anayo sababu ya msingi ya
kuishawishi mahakama impunguzie adhabu
Katika utetezi
wake mshitaki aliiomba mahakama impunguzie adhabu kwa kuwa anafamilia ya
wake wawili ambao wanamtegemea pamoja na watoto ombi ambalo lilipingwa na mwendesha mashitaka
Baada ya utetezi
huo hakimu Chiganga alisoma hukumu kwa
kueleza kuwa kutokana na mshitakiwa
Emanuel Philipo kupatikana na kosa hilo mahakama imemuhukumu kwenda jela
kutumikia kifungo cha miaka 30 jela kuanzia mei
26 mwaka huu
No comments:
Post a Comment