Friday, April 4, 2014

MKUU WA AKEMEA TABIA YA VIONGOZI KUKIMBILIA VIKAO VYENYE POSHO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Mkuu wa Wilaya  ya Mpanda Paza  Mwamlima  amekea  tabia ya viongozi wa Halmashauri ya Mji wa Mpanda kukimbilia  huhudhuria  kwa wingi kwenye vikao wanavyolipwa posho na kuvikimbia  kuhudhuria  vikao ambavyo hawalipwi posho
Mwamlima  alitowa kauli hiyo hapo juzi kwenye  mkutano wa wadau wa  uzinduzi wa  mchakato  wa uanzishwaji wa mfuko wa  Afya ya  jamii wa utoaji  huduma ya  matibabu kwa kadi TIKA  uliofanyika kwenye ukumbi wa idara ya maji
Alisema wakuu wa Idara  zilizopo kwenye  Halmashauri ya Mji wa Mpanda wamekuwa na  tabia ya kutohudhuria  vikao vinavyokuwa vimeitishwa   ambavyo wanajua  hawata lipwa posho
Alieleza     kushangazwa na  idadi kubwa ya  wakuu wa Idara wa Halmashauri  hiyo  jinsi walivyojitokeza kwa wingi  kwenye  kikao hicho  tofauti na   wanavyo  hudhuria  kwenye  vikao  vingine
Alifafanua kuwa   wakuu wa Idara wamehudhuria kwa  wingi  kwenye  kikao hicho kwa kuwa  wamejua  kikao hicho  kinamalipo ya  posho ya kikao
Alisema babia hiyo   ya kukimbilia kwenye vikao vyenye posho ni  vizuri  wakaiacha mara moja  kwani sio tabia  nzuri kwa viongozi  kukimbilia  vikao vyenye  malipo na  kuvikimbia  vikao  ambavyo havina  malipo
Hivi  karibuni Mkuu  huyo wa  Wilaya ya Mpanda  alikuwa na ziara ya  kutembelea kata  mbalimbali za Halmashauri ya  Mji wa  Mpanda  kwa lengo la kukagua miradi ya  maendeleo na kufanya  mikutano ya hadhara akiwa   anatakiwa kuwa na wakuu mbalimbali wa idara  lakini walikuwa wanajitokeza  wakuu wa idara wachache sana kwenye ziara hiyo
Hari  hiyo ya kutojitokeza kwa wakuu wa idara wachache  kwenye ziara hiyo ambayo ilikuwa  haina malipo yoyote   ilisababisha Mkuu  huyo wa Wilaya  akasirishwe  na  kitendo  hicho  ambapo kwenye  ziara yake ya  mwisho   mwishoni  mwa  wiki   iliyopita kwenye Kata ya  Makanyagio  alitaka kulazimika kutaka kuwaweka  mahabusu  wakuu wa  idara wote  ambao hawakuhudhuria ziara  siku  hiyo

No comments:

Post a Comment