Mtu mmoja
aliyefahamika kwa jina la Mele Seni (60) Mkazi wa Kijiji cha Kapalala
Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi ameuwawa kwa kukatwa
na panga kichwani na mgongoni na watu wasio fahamika wakati akiw
nyumbani kwake akiota moto
Kwa
mujibu wa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri
Kidavashari tukio hilo la mauwaji ya kinyama yalitokea hapo jana majira
ya saa moja na nusu usiku nyumbani kwa marehemu huyo kijijini hapo
Alisema
siku hiyo ya tukio marehemu akiwa nyumbani kwake amejipumzisha akiota
moto ghafla walitokea watu wasiofahamika na kupiga hodi nyumbani kwa
marehemu ambae nae aliwakaribisha watu hao kwa kujua ni watu wema
Alieleza
ndipo watu hao walipoanza kumshambulia marehemu kwa kumkata kwa panga
kwenye kichwa na mgongoni huku marehemu akiwa anapiga mayowe ya kuomba
msaada kwa majirani zake
Kidavashari
alisema licha ya marehemu kupiga moyowe majirani zake hawakuweza
kujitokeza mapema kuweza kumpatia msaada na ndipo watu hao walipoona
Mele Seni amefariki dunia walitokomea kusiko julikana
Majirani
waliweza kufika nyumbani kwa marehemu baada ya muda mrefu wa kutokea
kwa tukio hilo ambapo walimkuta marehemu akiwa ameisha fariki dunia huku
mwili wake ukiwa na majeraha ya panga kichwani na mgongoni na kisha
walitowa taarifa kwa uongozi wa serikali ya kijiji ambao nao walitowa
taarifa kwa jeshi la polisi
Kamanda
Kidavashari alieleza kabla ya tukio hilo marehemu alikuwa
akilalamikiwa na majirani zake na wanakijiji hicho kuwa amekuwa
akijihusisha na vitendo vya kishirikina kwa kuwaroga watu kijijini hapo
Hivyo
uchunguzi wa awali uliofanywa na jeshi la Polisi umebaini kifo hicho
kametokana na imani ya ushirikina ulisababisha wanakijiji hicho
kumjengea chuki marehemu huyo
Mpaka sasa hakuna
mtu au watu waliokamatwa kuhusiana na tukio hili na jeshi la
polisi linaendelea na upelelezi ili kuwakamata na kuwafikisha
mahakamani waliohusika katika tukio hili
Kamanda wa Polisi
wa Mkoa wa Katavi ametowa wito kwa wananchi kutojichukilia
sheria mkononi kutokana na kuwahusisha watu na imani za kishirikina na
matokeo yake wamekuwa wakiua watu pasipo sababu
N a Walter Mguluchuma
Mpanda Katavi
No comments:
Post a Comment