Home » » WAZIRI UMMY MWALIMU AZIAGIZA HALMASHAURI KUJENGA VITUO VYA AFYA KWENYE WATU WENGI.

WAZIRI UMMY MWALIMU AZIAGIZA HALMASHAURI KUJENGA VITUO VYA AFYA KWENYE WATU WENGI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Na  Walter  Mguluchuma .
       Katavi .
  Waziri wa  Afya   Maendeleo ya   jamii   Jinsia ,  Wazee na  Watoto  Ummy  Mwalimu    ameziagiza   Halmashuri  zote  hapa   nchini kuhakikisha   zinajenga  vituo  vya  Afya kwa  kuzingatia   geografia ya   eneo  husika na kuangalia  sehemu   ambayo wanaishi watu wengi .
Agizo  hilo    alilitowa hapo  jana     wakati  alipokuwa    akizungumza  na  viongozi  wa  Serikali wa   Mkoa  wa   Katavi   katika  ofisi ya   Mkuu wa   Mkoa wa    Katavi  mara  baada ya  kupokea taarifa ya  utekelezaji wa  shughuli za   Serikali za  Mkoa  huo.
  Alisema  Serikali  inampango wa  kujenga  zahanati  kwenye  kila  kijiji  na  Kituo  cha   Afya  kwenye  kila   Kata  ila  kwa  sasa  ni   vigumu  kwa  kila    Kata   kuwa  na    kituo  cha  Afya  kutokana  na   uhaba wa  wataalamu wa  afya .
Hivyo kila    Halmashauri  iangalie  uwezekano  wa  kufanya    kila   Kata   tatu kuunganisha  nguvu ya  pamoja  na  kujenga  kituo  cha  afya  kimoja  ambacho  kitatowa  huduma    kwa  wananchi  w  kata   hizo   tatu na   waangalie  geografia  ya  eneo  husika  na        pia   idadi ya  wingi wa  watu.
  Alionya  kuwa  ipo    tabia ya  baadhi ya  madiwani   watakao  taka     kituo     kijengwe   kwenye   Kata  yake  hata   kama    Kata  nyingine   ndio  inayokuwa   inasitahili  hivyo ni   vema  wakaa pamoja     madiwani  na  wataalamu wakashauliana  kwanza   sehemu  ambayo inafaa  kujengwa kwa kituo cha   Afya.
Kwa  upande  wake   Mkuu  wa   Mkoa   Katavi   Meja   Generali  mstaafu  Raphael   Muhuga   alieleza  kuwa   vituo  vya   kutolea  huduma  za  Afya     vimeongezeka  kutoka 72 kwa  mwaka  2012  hadi  vituo   84.
 Alisema  ili  kutekeleza   azma  ya  Serikali  ya  kila  Kijiji kuwa na  Zahanati   Kata  kuwa na   kituo  cha  Afya  na  Wilaya  kuwa na  Hospitali ya  Wilaya   Mkoa  wa  Katavi   katika  kutekeleza   mpango wa  maendeleo  ya  Afya  ya   Msingi  MMAM    imejenga  zahanati  21  toka  mwaka  2012    hadi  june   2017   hivyo  idadi  kuongezeka  kutoka    59  hadi  kufikia  Zahanati  70.
Nae  Asifa  maedeleo ya  Jamii  wa  Mkoa w  Katavi  Anna    Shumbi   alieleza  kuwa   Mkoa  huo  unakabiliwa  na  changamoto  kubwa  ya   mimba  za  utotoni  na   kuufanya   Mkoa huo   kuwa ni  miongoni  mwa  Mikoa  inayoongoza  kwa  tatizo la   mimba  za  utotoni .

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa