Home » » WAKRISTU NA WAISLAM WAMALIZANA

WAKRISTU NA WAISLAM WAMALIZANA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na    Walter  Mguluchuma
Katavi
Diwani wa Kata ya  Ntongwe Wilaya ya Tanganyika Mkoa wa  Katavi  Frenk   Kibigazi jana amefanikiwa kuutatua mgogoro wa kidini   baina ya wakristu na  Waislamu wa Kijiji   cha   Majalila uliokusababisha Sheikh Hamis Kakoti kunusurika kipigo kutokana na kauli aliyoitoa wakati wa mazishi ya mwislam ambayo ilitafsiriwa kuwa ni kejeli kwa wakristu.

Mgogoro huo ulitokea  wakati wa mazishi ya  baina  ya  waumini mazishi ya  mgambo   aliyekuwa  anaaminika  na  wakazi wa  Kata  hiyo Tano Nkuba ambae  mazishi yake yalikuwa yalifanyika  siku hiyo ambapo sheikh huyo alipokuwa akiwaasa waislamu aliwaambia kuwa "wasali sana wasiwe kama wakina John na Katabi ambao wanaabudu tu" kauli iliyowakwaza wakristu.
Baada ya kauli hiyo lilizuka zogo kubwa makaburini hapo hadi pale  Katekista wa   dhehebu  la  Katoliki  Credo  Lusambo  alipoingilia  kati na  kuwasihi  waumini wa kikristu wapunguze  hasira na kuwaahidi kuwa   na swala  hilo  litakwenda kumaliziwa  kwenye   msiba nyumbani kwa  marehemu.
Walipo  fika  nyumbani kwa  marehemu waumini wa dini ya Kikristu walidai kuwa  kuanzia siku hiyo hawako  tayari tena kushirikiana   na Waislamu  mpaka  hapo   Shekhe Kakoti atakapo waomba radhi kwani  lugha aliyoitumia ilikuwa ni ya kuwakashifu wakristu na imewaudhi kupita  kiasi.
 Hata  hivyo    Shekhe  huyo hakukubali  kuomba  msamaha  kutokana  na kauli yake   aliyoitoa  hari  ambayo iliwafanya   wakristu waondoke   msibani  hapo huku wakiwa  na  msimamo  wa kutoshirikiana  na   waislamu kwa  jambo lolote  lile liwe zuri  ama baya.
Baada ya siku kadhaa kupita ndipo diwani wa  Kata  ya  Ntongwe, Frenk  Kibigazi alisema haiwezekani mgogoro huo ukaachwa uendelee  kuwa ulivyo   hali iliyo mlazimu kuitisha mkutano ambapo alishirikisha  pande  mbili hizo  ili kutatua mgogoro huo wa  kidini uliokuwa  umetokea siku kadhaa zilizopita.
Katika mkutano huo diwani huyo alisema kuwa yeye kama kiongozi wa kata hiyo hayupo tayari kuona kunamgawanyiko na watu wakiishi bila kushirikiana kitendo ambacho ni kibaya  na sio utamaduni wa kitanzania kwani watanzania panapotokea jambo daima wamekuwa wakikutana na kulitatua ili maisha ya amani, mshikamano na ushirikiano yaendelee kama awali.

Baada ya mazungumzo ya muda mrefu viongozi  hao wa   dini  walikubaliana  kumaliza  tofauti zao na kukubaliana pia  kwenda  kwa waumini  wao makanisani na  misikitini kuwaeleza kuwa   mgogoro  uliokuwepo   umekwisha   hivyo    waendelee kushirikiana    kwenye  mazishi na  kwenye  mambo mengine kama kawaida na kuwaonya viongozi wa kidini kujiepusha na kauli  zinazoweza kukwaza upande mwingine kwani daima zimekuwa ni chanzo cha mifarakano katika maeneo mengi ndani na nje ya nchi yetu.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa