Home » » HALMASHAURI ZA AGIZWA KUTOWAMISHA WATU KABLA YA KUWALIPA FIDIA ZAO .

HALMASHAURI ZA AGIZWA KUTOWAMISHA WATU KABLA YA KUWALIPA FIDIA ZAO .

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


 Na  Walter   Mguluchuma .
      Katavi .
Naibu Waziri wa   Ardhi  Nyumba  na  Maendeleo ya   Makazi  Anjelina  Mabula  ameziagiza   Halmashauri kuacha  tabia ya kuwahamisha  watu  kwenye  Makazi  yao  wanayoishi  kabla ya kuwalipa   fidia .
Agizo  hilo  alilitowa   hapo  jana  kwenye mikutano ya hadhra iliyofanyika katika kata za Misunkumilona Nsemlwa  kwa   nyakati   tofauti  wakati    alipokuwa   akizungumza  na   wakazi wa   Kata  za   Nsemlwa    na   Minsukumilo   kwenye   mikutano  ya   hadhara    alipokuwa  akizungumza  na  watumishi wa   Wizara   yake  wa    Halmashauri  za    Mpanda ,  Nsimbo  na   Manispaa ya   Mpanda  kwenye  kwenye  ukumbi  wa   idara  ya   Maji   mjini   hapa .
Alisema  kumekuwepo na  tabia  ya  kuwahamisha   wananchi  kwenye  maeneo yao  wanayoishi  bila  kuwalipa  fidia  na  maeneo  hayo  kupimwa   viwanja  na  kupewa  watu   wengine .
Alisisitiza  kuwa   Serikali ya   awamu ya  tano   haiiko     tayari  kuona  wananchi  wanaondolewa  kwenye   maeneo  yao     waliokuwa   wakiishi  bila  kulipwa  fidia  kwani  kufanya  hivyo  ni  kuwanyanyasa   wananchi .
Naibu   huyo  Waziri  wa  Ardhi  alikemea  tabia   inayofanywa  na  watumishi  wa   iIdara ya      Ardhi  ya  kupima  maeneo ya    viwanja  na  kuwanyima  watu   ambao walikuwa   wakiishi  kwenye   maeneo  hayo  na  kuwapatia  watu   wengine  kwani  kufanya  hivyo ni  wizi  kwa  wananchi .
Hivyo  aliagiza  kuwa  maeneo  yote    ambayo  yatakuwa  yanapimwa  viwanja  wanaotakiwa  kupewa  kipaumbele  ni  wale  wananchi waliokuwa  wakiishi  kwenye  maeneo  hayo   baada  ya  hapo  ndipo  wepewe  watu  wengine .
Pia   ameziagiza    Halmashauri  kuhakikisha  zinapima   viwanja  na mashamba kisha kutoa hati miliki za viwanja  na kuwapatia wananchi hati hizo ziweze kuwasaidia katika  kuomba hata mikopo kwenye taasisi za mabenki.
Pia hati hizo zitasaidia kupunguza migogoro ya watu wanaovamia maeneo ya taasisi za umma.
Na kuondoa migogoro ya ardhi ambayo imekuwa ikitokea matra kwa mara. Kwenye maeneo mengi hapa nchini.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa