Home » » MAKAMU WA ASKOFU AWATAKA WATU KUZAA WATOTO WATAKAO WEZA KUWATUNZA.

MAKAMU WA ASKOFU AWATAKA WATU KUZAA WATOTO WATAKAO WEZA KUWATUNZA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


         Na  Walter    Mguluchuma .
                                Katavi .
  Makamu wa  Askofu wa  Kanisa  Katoliki  Jimbo la  Mpanda  Padri  Patrick  Kasomo amewataka watu waache  tabia ya kuzaa  watoto wengi na   badala yake  wazae watoto  ambao wataweza kuwatunza kwa kuwapatia mahitaji yao ya muhimu.

Wito huo   aliutowa  hapo jana  wakati wa  mafunzo ya viongozi  mbalimbali wa Dini wa Kanisa   hilo   yaliondaliwa  na  Taasisi  ya   Benjamin    Mkapa   Foundation  na  yaliofanyika  katika  ukumbi wa  Chekechea   Mjini  hapa  yaliokuwa  na lengo la kuwaelimisha   watu kujikinga na kujiepusha na Ukimwi.

  Alisema  watu watu wamekuwa  na  tabia ya kuzaa  watoto wengi  bila   mpangilio na  matokeo yake wakuwa wakishindwa kuwatunza  watoto hao  kutokana  na kuwa  na  uchumi   mdogo wa kipato .
Makamu  huyo wa  Askofu  alieleza      familia  nyingi    za  watu   maskini   ndio   zinaongoza  kwa   kuwa  na idadi kubwa ya  kuzaa  watoto wengi  kuliko watu  wenye  uwezo wa kiuchumi .
Alisema  watu  ambao wanazaa  watoto wengi  matokeo yake  watoto  hao   wanakuwa   hawana   akiri  darasani   hivyo  ni  vema  watu  wakazaa  watoto  ambao wanaweza  kuwatunza .
Pia    aliwataka  watu  wajenge tabia  ya kupima   afya  zao  na  wawe  waaminifu  kwenye  ndoa zao  na  wasiige    utamaduni wa  Nchi   nyingine  ambao  umekuwa ni  chanzo   cha wtu  kuacha  kufuata   mila  na utamaduni  wa   Nchi yetu .
 Afisa  mradi  wa TB   na  HIV   wa   Taasisi ya   Benjamin  Mkapa   Magiri  David  alisema Taasisi ya   Benjamin Wiliam  Mkapa  kupitia   Save   the   Children   imepokea  ufadhili  kutoka  mfuko  wa  Dunia  wa kupambana  na maambukizi  ya kifua kikuu  TB ,virusi vya  ukimwi  VVU  na  Malaria  ambao utatekelezwa  kwa muda wa miaka miwili.
 Taasisi hiyo  kwa kushirikiana  na  Wizara   ya  Afya , Maendeleo  ya jamii Jinsia Wazee  na Watoto  kupitia   mpango  wa Taifa  wa kuratibu  huduma za  UKIMWI  umetowa  mafunzo  hayo  kwa viongozi wa  dini  ya  kuhusu  elimu  juu ya  maambukizi ya Ukimwi.
Magiri  alisema   baada ya kupatiwa  elimu  hiyo  viongozi hao wa Dini wanategemewa kuwa watakuwa  mabalozi  wazuri katika jamii kwa kuweza kufikisha  elimu  walioipata kwa jamii inayowazunguka  ili kupunguza  maambukizi  ya VVU  na pia wao wenyewe kujikinga  na maambukizi ya VVU .
Mafunzo  hayo  yatatolewa  katika Mikoa ya   Tabora na   Rukwa  na yatawafikia  waumini  wa madhehebu ya  Dini mbalimbali  wasiopungua 500 hadi kufikia  Desemba mwaka huu.
Nae    mkufunzi wa    mafunzo  hayo  kutoka     Benjamin  Mkapa   Foundation  Peter  Nyambo  alieleza  kuwa  umefika wakati sasa  kwa  watoto wadogo kuelimishwa  ili  waache kufanya   tendo  la  ndoo  wakati wakiwa  na  umri  mdogo .
Tabia ya  watoto  kuanza  kufanya  tendo la  ndoo kumekuwa  kukichangia  watoto hao kupata  maambukizi ya VVU   kutokana  na  kutojua  kujikinga   na   maambukizi ya  VVU.
  Alisema  Taasisi ya  Benjamin  Mkapa     Foundation  imeamua  kuwapatia  mafunzo   viongozi    wa  madhehebu  mbailimbali  ya  Dini   ili na  wao  waende  wakatowe   elimu  kwenye  makundi  mbalimbali       juu ya   kujikinga  na    maambukizi ya  VVU .
Alifafanua   kuwa    Taasisi  hiyo imepanga  kuendelea  kutowa  elimu  iliifikapo  mwaka  2030   maambukizi  ya VVU  yawe  yamekwisha   kabisa   hapa   Nchini  Tanzania .
Mratibu  wa    Ukimwi  wa   Halmashauri ya  Wilaya ya  Mpanda   Kasara   Bulemo  alisema     Wamejipanga  kufika  kwenye   Kata   zote 16 za  Halmashauri  hiyo  ili kutowa   elimu  ya kupima   maambukizi ya  VVU  kwa  hiari .
 Alisema   maambukizi ya  VVU    katika   Mkoa wa  Katavi  ni  5.9 na   yamekuwa   yakichangiwa  sana kwenye   maeneo ya   mikusanyiko ya  watu  hasa   wakati wa  msimu wa  mavuno .
Aliyataja  baadhi ya  maeneo  yenye   maambukizi   mengi ya   VVU  katika  Halmashauri ya   Wilaya ya  Mpanda  kuwa  ni   Karema , Ikola ,  Mnyagala  na   Kasekese.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa