Home » » HATARI NYUMBA ZAPAKWA DAMU INAYOSADIKIWA KUWA NI YA MNYAMA AU BINADAMU KATIKA KUTA NA MILANGO YA NYUMBA , WANANCHI HASHIKWA HOFU

HATARI NYUMBA ZAPAKWA DAMU INAYOSADIKIWA KUWA NI YA MNYAMA AU BINADAMU KATIKA KUTA NA MILANGO YA NYUMBA , WANANCHI HASHIKWA HOFU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



Na Walter  Mguluchuma

      Katavi

WAKAZI wa  Kata ya  Nsemlwa iliyoko katika  Manispaa ya  Mpanda
katika mkoa wa Katavi   wanalazimika  kulala  mapema kutoka na
kushikwa  na  hofu   baada ya  milango na kuta za  nyumba  wanazoishi
kupakwa  damu inayodhaniwa kuwa ya binadamu au mnyama

Nyumba za  Ofisa Mtendaji wa Kata ya Nsemlwa na Mwenyekiti wa Mtaa wa
Nsemlwa  ni miongoni mwa nyumba 300 zilizopo katika mitaa yote mitano
ya kata hiyo zinazodaiwa kupakwa damu hiyo.

Akizungumza na gazeti hili Ofisa Mtendaji wa Kata hiyo , Jumbe Mselwa
alisema tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia Jumapili  ambapo watu
wasiofahamika walipaka nyumba hizo damu  na kusababisha hofu kubwa kwa
wakazi wa eneo hilo.

Alisema   taarifa za mkasa huo   zilifikishwa  ofisini  kwa ke  na
wenyenyeviti wa  wa  serikali za mitaa   mitano ambapo alilazimika
kwenda kuhakikisha   na  kukuta  nyumba  hizo  zikiwa  zimepakwa  damu
 nje  na  nyingine  ndani.

Jumbe  aliitaja  mitaa   hiyo  ambayo  nyumba  zake  zimepakwa   damu
kuwa  ni   pamoja na     Mtaa   Kichangani ,  Migazini ,Kilimani
Tulieni  na  Mtaa  wa   Nsemlwa   ambao  ndio  unaongozwa  kwa  nyumba
     nyingi kupakwa  damu .

‘Nimewataka   wakazi wa kata hiyo    mara  wanaopoona  kitu   ambacho
sio   cha  kawaida   watoe   taarifa  mapema  kwa  uongozi  wao wa
mitaa  wanayoishi “ alisisitiza .

Kwa upande wake Mwenyekiti wa  Mtaa wa  Nsemlwa ,   Adamu   Masigati
alikiri kwamba    nyumba  yake  ni  miongoni   mwa    nyumba   ambazo
 zimepakwa  damu usiku huo ambapo   n wakazi wa mtaa huo wanahoji
kulikoni   tukio  hilo  litokee usiku   badala ya    mchana .

Msagati   alieleza  kuwa jana alitaarifiwa kuwa   m  wa  Mtaa  huo
mkazi  wa mtaa huo alidondokewa na  matone  ya damu hiyo wakati
alipokuwa ndani ya nyumba yake akila chakula cha usiku .

Akisimulia    mkasa huo mkazi huyo aitwae ,    Raphael   Geoge   juzi
akiwa  nyumbani  kwake   saa  kumi  jioni akila  chakula   sebuleni
kwake ambapo  alipoanza kula   tonge  la  pili  la ugali  ghafla
aliona  matone  mawili ya  damu  yenye  ukubwa    wa  sarafu ya
shilingi  100 yakidondoka  alipokuwa  amekaa .

Alisema  tukio hilo  ilimshitua  ambapo alimwaita  binti yake aitwae
Maliselina   Joseph ili   nae   ashuhidie  damu  hiyo     ambayo
haikufahamika  imetoka  wapi .

Umati  mkubwa  wa watu  walifurika nyumbani kwa Raphael ambapo
walishtushwa baada ya kushuhudia  nzi  wakiwa wamerundikana kwenye
matone ya damu  hiyo ambapo walitoa taarifa kwa uongozi wa Serikali ya
Mtaa wa Nsemlwa.

  Mkewe   Raphael   aitwaye    Judith  Joseph   ambae   wakati wa
tukio  hilo  hakuwepo  nyumbani  anasema  aliporudi  nyumbani   saa
moja  na  nusu  usiku  alikuta   familia  yake  wakiwa  wamekaa  kama
wagonjwa.

  “ Nimemshauri mume wangu tuhamie kwenye nyumba nyingine lakini
amekataa akisisitiza kuwa ingekuwa ni nyumba ya kupanga angehama
lakini hawezi kwa kuwa ni nyumba yake aliyoijenga mwenyewe ….sasa ni
siku mbili zimepita nimeshindwa  kufanya usafi wa nyumba kwa ajili ya
woga isitoshe sasa tunalazimika kulala mapema kabla ya saa mbili
usiku” alieleza.



 Kwa upande wake   Wasitala  Ferusi  alisema   yeye  na    familia
yake  tangu   nyumba yao ilipopakwa  damu  wamekuwa wakijifungia  na
kulala  mapema   huku  akiwazuia watoto wake  kutembea  hata kwa
majirani .

Alisema kinachostaajabisha wengi damu hiyo imepakwa kwenye kuta  ndani
ya nyumba  huku milango ikiwa imefungwa usiku

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa