Home » » HATARI: JELA KIFUNGO CHA MAISHA KWA KUMLAWITI MTOTO MWENYE UMRI WA MIAKA 9. KWENYE JIKO LA KUCHOMEA TUMBAKU

HATARI: JELA KIFUNGO CHA MAISHA KWA KUMLAWITI MTOTO MWENYE UMRI WA MIAKA 9. KWENYE JIKO LA KUCHOMEA TUMBAKU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



     Na  Walter  Mguluchuma .
                         Katavi .
Mahakama ya  Wilaya ya  Mlele  Mkoa wa  Katavi  imemuhukumu    Mkazi wa  Kijiji cha Ilunde   Tarafa ya  Inyonga  Wilaya ya  Mlele Mkoani  Katavi   Festo  Joseph  29 adhabu ya  kifungo cha   maisha  jela  baada ya kupatikana  na  kosa  la kumlawiti  mtoto  wa kike  mwenye umri wa miaka tisa .
  Hukumu  hiyo  ambayo iliwasisimua watu  wengi wa  Wilaya ya  Mlele ilitolewa  hapo  jana  na  Hakimu  Mkazi wa  Mahakama ya  Wilaya ya  Mlele   Theotimus  Swai  baada ya mshitakiwa  kukiri Mahakamani hapo kuwa ni kweli  alimlawiti mtoto  huyo wa kike.
Awali  Mahakamani  hapo  mwendesha  mashitaka   mkaguzi  wa jeshi la  Polisi   Baraka  Hongoli alidai Mahakamani  hapo kuwa   mshitakiwa  Festo  alitenda  kosa  hilo  hapo  Novemba  10 katika  Kijiji  hicho cha  Ilunde .
 Siku hiyo ya  tukio  mshitakiwa  alifika  nyumbani kwa wazazi wa mtoto huyo  na kumdanganya  mtoto huyo  kuwa  baba yake  ambae hakuwepo  nyumbani  nyakati  hizo za   saa  sita  mchana  kuwa  alimtuma  akamwonyeshe   nyasi  alizokata  kwa  ajiri ya kuenzekea    nyumba  yao  katika  moja  ya pori  Kijijini  hapo .
Mwendesha  mashitaka  Hongoli    alidai  kuwa  baada ya mtoto kukubali  kuongozana  na  Festo   hadi  katika  pori  hilo  ndipo  alimkamata  na kumpeleka  hadi  katika   Bani moja  la jiko la kukaushia  tumbaku   ambapo  aliingia  nae   na kisha  alimfanyia kitendo hicho cha kumlawiti  bila  kujari mayowe ya mtoto huyo  aliyekuwa akipiga kuomba msaada  kutokana  na  maumivu  makali   aliyokuwa  akiyapata  katika  sehemu zake .
Mshitakiwa  huyo baada ya kuwa   amemfanyia  unyama huo   wa kumlawiti  kisha  alimrudisha   hadi   karibu   na nyumbani  kwa wazazi wake  huku  akimtishia kuwa  asitowe  siri  hiyo kwa mtu yeyote Yule  vinginevyo  akifanya  hivyo  atamuuwa .
Baada ya   kufika  nyumbani  nyumbani kwao  mtoto huyo  alianza kulia  akilalamika  maumivu  makali  aliyoyapata  ndipo wazazi wake  walimuuliza  analia nini  ndipo alipowaeleza   yaliomfika  huku  akimtaja  muhusika  wa kitendo  hicho  ambapo  mbiu ilipigwa Kijijini  hapo  na kikosi cha  Sungusungu kilianza kazi ya kumsaka  kijana  huyo Festo  kwenye kila  kona  ya  Kijiji  na kufanikiwa  kumkamata  majira ya saa 12 jioni  akiwa  amejificha  porini .
  Hongoli  aliambia   Mahakama   mshitakiwa  huyo  wakati  akiwa mikononi mwa   Sungusungu  walimrejesha  Kijijini  hapo    Festo  alikiri kutenda kosa  hilo  huku akiwaomba wakazi wa Kijiji  hicho  msamaha  hata    hivyo wananchi  hao  hawaku mwachia  na walimpeleka  hadi  kwa   Mtendaji wa  Kata  ambapo   alikiri tena   kutenda kosa  hilo na  ndipo  alipochukuliwa  na kufikishwa kituo  cha  Polisi   Inyonga   alikiri kwa  maneno na   maandishi kuwa alimlawiti  mtoto  huyo .
Mshitakiwa   katika  utetezi wake  Mahakamani  hapo   aliiomba   Mahakama   hiyo impunguzie    adhabu kwani   katika   maisha yake   alikuwa  hajawahi  kutenda kosa   kama  hilo   hata  hivyo   Hakimu  Swai  alimukumu  kifungo cha   maisha  jela  huku akiongeza kuwa  kosa  hilo   halina   adhabu  mbadala zaizi ya kifungo cha  maisha  jela .

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa