Home » » WANAOFANYA UJANGILI WAAGIZWA KUACHA NA KUTAFUTA KAZI NYINGINE YA KUFANYA

WANAOFANYA UJANGILI WAAGIZWA KUACHA NA KUTAFUTA KAZI NYINGINE YA KUFANYA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


    Na   Walter  Mguluchuma .
     Katavi .
   Serikali  imewaagiza  watu  wote  wanaofanya  shughuli za  ujangili kuacha mara  moja na watafute   kazi  nyingine ya kufanya  kwani    kwa sasa  huko  porini  hakukaliki  na  Serikali  itawasaka popote  pale walipo hata kama ni nje ya Nchi na kuwakamata  watu  wote   wanaofanya  ujangili bila kujari cheo  cha mtu na .
 Agizo  hilo  la   Serikali  lilitolewa   hapo  jana   na    Waziri   wa  Maliasili    na  Utalii  Prof   Jumanne    Mghembe  wakati  alipokuwa  akifunga  mafunzo  ya ukakamavu  kwa  Wahifadhi  wa  Wanyama  Pori  kutoka   Tanapa , Mamlaka ya  Ngorongoro  na  Tawa  yaliofanyika  katika  kituo  cha     mafunzo cha  Mlele   Mkoani    Katavi .
 Alisema   agizo    kwa   majangili    wanaofanya   ujangili  waache kufanya  kazi  hiyo  na watafute  kazi  nyingine  ya kufanya  kwani  Serikali  itawasaka  huko  huko  waliko  hata  kama  ni nje ya   Nchi  na wala  hawata   jari i cheo cha  mtu  na wajukuwe  kuwa   sasa hivi  porini  hakukaliki  tukana   na  Wizari  ilivyojizatiti  katika  kulinda  rasimali za   nchi .
 Waziri  Mghembe  alieleza   katika  kipindi  cha   mwezi  Agosti  hadi   Oktoba  mwaka huu  majangili  107 walikamatwa   hapa  Nchini  wakiwa na  nyara  mbalimbali  za   Serikali    pamoja  na   silaha  kutokana  na  kuwepo kwa  uporesheni   Faru
 Alisem   Serikali   itaendelea   kutekeleza    mkakati  wa  Kitaifa  wa kupambana   na ujangili  na biashara   haramu  ya  wanyama   na  nyara  za   Serikari    National    Strategy to  Combat   Poaching  and   lllegal   wildlife    Trade  pamoja  na  mambo  mengine   mkakati  unataja   umuhimu  wa kuwapatia   mafunzo  wahifadhi  wanyama  pori  yatakayo wawezesha  kufanya  kazi kwa ufanisi zaidi .
 Jitihada   zitaendelea  kufanyika   na kuhakikisha   kwamba   kila   furusa  ya    mafunzo  inayopatikana  inatumika   vizuri  ili kuwajengea  uwezo  watumishi  kwa kuwapatia   mbinu   za   teknojia  ya kisasa  katika  kupambana  na  ujangili .

 Wizara ya  Maliasili   na  Utalii   itaendelea  kushirikisha  wadau  mbalimbali   kutoa  mafunzo ,vitendea  kazi  na  teknojia ya kisasa  itakayorahisisha  kuwabaini  na   kuwakamata   majangili   ndani  au nje  ya  maeneo yaliyohifadhiwa .
  Alisema   sekta ya  Uwifadhi  imeanza  kutumia  ndege   zisizo  na   rubani   DRONES   kubaini   majangili  katika   baadhi  ya    maeneo  ya   hifadhi   hapa  nchini  na  matumizi ya   mbwa  wa kunusa  katika  kufutilia   majangili  na  katika  ukaguzi wa  nyara  za  Serikali .
Alieleza  kuwa  maeneo  mengi  ya    hifadhi   yanakabiliwa  na    changamoto   mbalimbali    zikiwemo  ujangili  hususani   wa  Tembo , uingizaji wa   mifugo   hifadhini  ,uvamizi  wa  mipaka ya  hifadhi  na  uwelewa   mdogo wa   wananchi .
Nae  mwakilishi   wa Mkurugenzi   Mkuu wa  Tanapa   Mtango    Mtahiko   alisema   Tanapa  wamekuwa  wakifanya  kazi  kwa  kutekeleza   maagizo ya  Wizara    ya  Maliasili na   Utalii na  watendelea  kufanya  hivyo  ili  kulinda   uhifadhi wa   Nchi .
Kaimu  Mkurugenzi  wa  TAWA     Martini  Loibooki  alisema   mafunzo  hayo waliopatiwa  Wahifadhi  hao yanaumuhimu   mkubwa    sana  kwani  wao  ndio   wasimamizi wa   askari na  watahakikisha  watumishi  wote wa  Tawa   wanapatiwa  mafunzo  kama    hayo kwani  yanawaongezea   ukakamavu na  uwezo wa kupambana  na   majangili .
MWISHO


    

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa