Home » » WANAFUNZI WATUMIA CHUMBA KIMOJA ZAIDI YA MADARASA MAWIL NA WENGINE WANAKAA CHINI..

WANAFUNZI WATUMIA CHUMBA KIMOJA ZAIDI YA MADARASA MAWIL NA WENGINE WANAKAA CHINI..



  Na   Walter   Mguluchuma .
         Katavi .
   Wanafunzi wa  Shule ya    Msingi   Kawanzige   katika  Manispaa ya  Mpanda   Mkoa wa  Katavi wanalazimika  kutumia    chumba   kimoja  cha   darasa  zaidi ya  wanafunzi  wa  madarasa  mawili kwa  ajiri ya kufundishiwa  masomo kwa wakati  mmoja  kufutia  shule  hiyo  kukabiliwa na  uhaba  mkubwa wa  upungufu wa  madarasa huku  wanafunzi wengine wakiwa wanasomea  chini.
  Kilio  hicho cha  wanafunzi wa  madarasa  zaidi ya   mawili  kusomea  katika   chumba  kimoja kwa  wakati mmoja  kilitolewa  hapo  juzi  na   Diwani  wa  Kata  ya  Kakese  Mh   Maganga   Salaganda  wakati wa kikao cha  Baraza  la   madiwani wa  Manispaa ya   Mpanda   kilichofanyika  katika   ukumbi wa  Mnspaa  hiyo .
 Alisema   shule ya  Msingi ya   Kawanzige  ambayo  ipo  kwenye  Kata  yake  inakabiliwa  na   changamoto kubwa ya  upungufu wa   madarasa    hari   ambayo  inaifanya   shule  hiyo   yenye   Wanafunzi wa  kuanzia     darasa  la  awali  hadi  la   saba  wanafunzi kutumia  darasa  moja   kwa  ajiri ya  masomo wanafunzi wa   madarasa zaidi ya  mawili  na  wote wamekuwa wakifundishwa kwa wakati mmoja .
 Aliiambia    Baraza  hilo la    Madiwani    lilikuwa   likiongozwa  kwenye   kikao   hicho na   Meya  wa  Manispaa ya    Mpanda   Willy   Mbogo  kuwa  shule   hiyo  yenye   Wanafunzi  zaidi ya   mia  sita  inayo  madarasa   manne  tuu.
Hivyo  kutokana  na  uhaba  wa  vyumba  vya    madarasa   wamelazimika  kutoyachukua  madawati  ambayo  yamechangwa  na   wananchi  kwa kuwa   hakuna   vyumba  vya   madarasa vya kuyahifadhia madawati huku  baadhi ya   wanafunzi wakiwa  wanasomea  chini.
  Afisa   Elimu  wa  Manispaa ya  Mpanda    Vicenti   Kayombo   alikiri    kuwepo  kwa  tatizo la   upungufu   mkubwa wa  madarasa  kwenye   shule  hiyo.
  Alifafanua  kuwa   mahitaji ya   shule   hiyo  ni   madarasa   24  lakini  yaliopo  hadi   sasa  ni   madarasa   manne  hivyo   shule   hiyo  inaidadi ya  upungufu  wa   madarasa  ishirini.
Katika   mwaka huu wa  fedha    wa  2016 na  2017  Manispaa  hiyo  imetenga   fedha  kwa    ajiri ya  ujenzi wa  vyumba   tisa  vya   madarasa  na   kati ya   vyumba   hivyo   viwili   vitajengwa  katika   shule   hiyo ya   Msingi   Kawanzige  hivyo  inabakiwa  na  upungufu wa  vyumba     18  vya  madarasa.
  Kayomba  aliwataka   Madiwani  wa  Manispaa  hiyo  waendelee kuwaelimisha  wananchi  umuhimu  wa kuchangia  ujenzi wa  vyumba  vya  madarasa, nyumba za  walimu   , matundu ya  vyoo  na   madawati .
Nae  Diwani  wa  Kata  ya   Makanyagio   Haidari    Sumry alilalamikia  kitendo  cha   madiwani wa   Manispaa  hiyo kutokuwa  na  ofisi zao  kwenye   Kata  wazoziongoza .
 Alisema  badala ya  shughuli  zao  za  kuwahudumia  wananchi  kuzifanyia  ofisini   wanalazimika    shughuli  hizo  kuzifanyia   kwenye  nyumba  zao  kitu   ambacho sio  sahihi.

Ajibu  hoja  ya  Diwan   huyo   Mkurugenzi wa  Manispaa ya  Mpanda   John   Nzyungu  alisema   watajitahidi  kukamilisha  ujenzi wa    ofisi  za  madiwani kwa  awamu  awamu kwani  manispaa hiyo  haina  uwezo wa kukamilisha  ujenzi wa  ofisi  hizo kwa  wakati  mmoja

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa