Home » » WANACHAMA WA KATAVI WASEMA HAWAMTAMBUI PROFESA LIPUMBA KAMA MWENYEKITI WA CHAMA HICHO.

WANACHAMA WA KATAVI WASEMA HAWAMTAMBUI PROFESA LIPUMBA KAMA MWENYEKITI WA CHAMA HICHO.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na   Walter Mguluchuma .
   
   
Katavi


WANACHAMA wa CUF mkoani Katavi wametangaza  kuwa  hawamtambui  Profesa
Ibrahim Lipumba  kama mwenyekiti  halali wa chama  hicho.

.

Msimamo  huo  wa wanachama  hao  wa CUF  ulitangazwa na Mwenyekiti  wa
CUF wilaya ya Mpanda  mjini , Alam Ndimubenya katika mkutano  na
waandishi wa  habari  uliofnyik mjini hapa leo.

Alisisitiz kuwa  mwenyekiti wa CUF  katik ngazi ya wilaya  iliyoko
mjini  anatambulika  kama  mwenyekiti  wa  mkoa  husika .

Akifafanua alieleza kuwa  mkutano mkuu  wa dharura  ulitishwa na CUF ,
Agosti 21, mwaka  huu  ukiwa ajenda  mbili  ikiwemo ya kuridhia  Prof
Lipumba  kujiuzulu  Uenyekiti  wa Taifa  wa chama hicho .

“Ajenda nyingine ilikuwa  uchaguzi wa  Mwenyekiti  , Makamu Mwenyekiti
 wa Taifa  na wajumbe  wanne  wa  baraza  kuu la uongozi wa CUF
Taifa…. Lakini  baadhi  ya wajumbe wachache  walimuingiza kwa  nguvu
Profesa Lipumba  na kufanya fujo  iliyosababisha  mkutano huo
kuvunjika” alieleza .

Aliongeza kuwa  wajumbe hao  wachache walifanya vurugu  hiyo baada  ya
 wajumbe 476  wa  mkutano huo mkuu  wa dhrura sawa na  asilimia  70 ya
akidi walilidhia  kujiuzulu kwa Profesa Lipumba.

“Wananchi  wamekuwa wakizungumza  tofauti na  iliyokuwa   kwa
kutoelewa  mamlaka  ya  Msajili wa Vyama vya Siasa   kwa  hatua yake
ya kumtambua Profesa Lipumba  kama  mwenyekiti wa CUF Taifa… basi  ni
vema  waelewe kuwa  mamlaka yake  yanishia  katika  kuvisajiri  vyama
vya  siasa  na si  vinginevyo “ aliongeza  kusema .

Alisema kuwa  sheria ya  vyama vya siasa  namba 5 ya 1995 toleo  la
2015 ikieleza  wazi  katika kifungu cha 20  juu ya mamlaka  ya Msajili
wa Vyama vya Siasa  kwamba  yanishia katika  kuvisjili vyama vya
siasa.
 
Hivyo  wanamuomba   msajili wa  vyama  vya  siasa   asijiengize  kwenye   mambo ya  CUF  kwani  matatizo ya  CUF  yatawalizwa  na  wanachama wenyewe wala si Msajiri wa  vyama vya  siasa. alisema   Mwenyekiti Dimubenya

Mwisho

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa