Home » » MWALIMU Mkuu wa Shule ya Msingi Msakila aahidi kujiuzuru endapo Shule yake haitakuwemo katika kumi Bora matokeo ya Darasa la Saba Kitaita

MWALIMU Mkuu wa Shule ya Msingi Msakila aahidi kujiuzuru endapo Shule yake haitakuwemo katika kumi Bora matokeo ya Darasa la Saba Kitaita


Na  Walter Mguluchuma .
     Katavi .


MWALIMU Mkuu wa Shule ya Msingi Msakila, Manispaa ya Mpanda mkoani
Katavi , Didas Makona  ameaapa  kuwa endapo shule yake  ispokuwemo
kwenye kumi  bora   ya  shule zitakazoongoza Kitaifa  katika matokeo
ya Kitaifa ya  kuhitimu Elimu ya Msingi  mwaka huu , atajiuzulu  kwa
hiyari  wadhifa wake .

Akisisitiza kuwa  itakuwa  fedheha  kubwa  kwake  na haoni  sababu kwa
nini  shule yake hiyo  ishindwe kuwemo  kwenye  orodha ya shule  za
msingi  kumi bora  katika matokeo  ya Kitaifa ambayo  yanatarajiw
kutangazwa  baadae  mwaka  huu.

Mwalimu  huyo alijigamba hiyo  alipokuwa akizungumza na waandishi wa
habari  leo , ofisi  kwake  shule hapo  katika Mtaa wa Kawajense ,
Manispaa ya Mpanda ..

Nimekuwa  Mwalimu Mkuu wa shule hii  kwa miaka mitatu sasa
nimewajengea  misingi  mizuri kielimu  wanafunzi  wanaosoma katika
shule  hii ambao  wana nidhamu ya hali ya juu …..” alisisitiza .

Akifafanua  alieleza kuwa  mwaka  2012  ufaulu  wa  kuhitimu elimu ya
msingi katika shule hiyo  ulikuwa asilimia 52 .

“Mwaka  2013  nilihamia  katika shule hii  na ufaulu  ulikuwa
asilimia  76  mwaka  2014  asilimia 92  na mwaka  jana  ufaulu
ulikuwa  aslimia 100…… kwa matokeo hayo  mwaka  jana kimkoa  shule hii
 ilishika nafasi  ya kwanza  huku  kitaifa  ilikuwa  ya  200 “
alisisitiza

Alisisitiza haoni  sababu itakayo  ifanya  shule  hiyo kutokuwa kuwa
kwenye kumi  bora  kutokana  na  jinsi  ambavyo  amewaandaa wanafunzi
wake 76  waliohitimu  elimu ya msingi mwaka  huu..

Sababu  nyingine   aliitaja  kuwa ni uwezo  waliokuwa  nao  wanafunzi
wake katika   masomo ya  Hisabati na Kingereza  ambapo kwenye
mitihani  sita ya  majaribio iliofanyika  kimkoa  robo ya  wanafunzi
76  walipata  alama  A ya ufaulu  , huku  waliobaki wote  walipata
alam a B wanafunzi wake robo ya   darasa wamekuwa wakipata  alama  B
ya ufaulu..

Alitamba kuwa  mtihni  huo  wa mjaribio  wanafunzi  hutumia dakika 45
kufanya    masomo  hayo ya  Hisabati na  Kingereza huku  muda wa
kitaifa ni saa mbili  huku akisisitiza kuwa  wanafunzi waliohitimu
daras la saba mwaka huu  walikuwa  wakijitungia  maswali  wenyewe  na
kutafuta  majibu wenyewe .

.Alisema  uwezo  huo walioonesha  ni  vigumu sana  kufanywa na
wanafunzi  kwani  kazi  hizo  zimezoeleka  kufanywa  na walimu  wao

Afisa  Elimu wa  Manspaa ya  Mpanda  Vicenti  Kayombo  alisema  mwalimu  Mkuu  huyo  alishafika  ofisini  kwake   na  alimwomba   amvue wadhifa wa  ualimu  Mkuu  indapo  shule  hiyo haitakuwa  kwenye  shule  kumi  bora kitaifa na  amwamishe  kwenye shule  hiyo na kumpangia kituo  kingine  cha  kazi  huku  akiwa ni  mwalimu wa  kawaida..

Mwisho



0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa