Home » » Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mhando amevunja bodi ya chama cha ushirika wa wakulima wa tumbauku

Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mhando amevunja bodi ya chama cha ushirika wa wakulima wa tumbauku

Na  Walter  guluchuma .
      Katavi
Mkuu wa Wilaya ya Tanganyika Salehe Mhando  amevunja bodi ya chama cha ushirika wa  wakulima wa tumbauku mishamo  kuagiza kukamatwa kwa viongozi wa bodi, mkandarasi aliyehusika kupewa kandarasi ya kupanda miti, Afisa Ushirika,kamati ya miti ya mkoa  na wale wote waliohusika na upotevu wa fedha  zaidi ya shilingi milioni 142 zinazodaiwa kupotea kwa kumlipa mzabuni alipewa zabuni ya kupanda miti kati kampuni ya Mtuka Investment inayomilikiwa na Moses Christopher Fred kwa ajili ya Kupanda  miti  3,25000 yeye alipanda miti 74,000 tu katika vijiji vya Tarafa ya Mishamo kwa ajili ya  wakulima watumbaku mishamo,   Mkoani Katavi.
Mkuu wa Wilaya alifikia hatua hiyo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wakulima tumbaku wa Tarafa ya Mishamo kuhusu ushirika wao wa  wakulima wa Tumbaku TAMCOS viogozi kutuhumiwa kuwadhurumu wakulima kwa kuwakata fedha za mauzo ya zao la tumbaku na kumlipa mkandarasi ambaye hakutekeleza wajibu wake ipasavyo.
Kufuatia kupokea malalamiko hayo Mkuu wa wilaya aliunda tume iliyopita kuhesabu miti  kwa kila kijiji kilichoelezwa kuwa miti ilipandwa kumbe haikupandwa,ililipwa miti hewa,hivyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika mishamo mkuu wa wilaya alitoa maamuzi kuhusu malalamiko ya wakulima hao.
Akifafanua Zaidi alisema kuwa kazi aliyowaahidi wananchi kuwa atahakikisha kazi anaifanya kuona jasho la munyonge halipoei.amlisema hela iliyokuwa ikilalamikiwa na wananchi ilikuwa shilingi milioni 142.iliyolipwa kwa mkandarasi mtuka kwa kupanda miti ambayo haipo.
Akizungumza kuhusu afisa ushirika ambaye ndiye jicho lake la kwanza alipomwulizakuhusu kama miti imepandwa kwa kuwa anasikia harufu ya wizi kuhusu upandaji miti kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2014/2015 chama cha ushirika tamcos,pia akamwagiza kushughulikia malalamiko ya pesa za masawazisho hakuweza kumpatia majibu ya kuridhisha.
Kufuatia malalamiko hayo  akaagiza kukamatwa kwa Mkandarasi husika mtuka Investment,bodi ya chama cha ushirka mishamo,Kamati ya Miti na Afisa ushirika na kuwataka fedha zilizopotea shilingi milioni 142 zirejeshwe baada ya hapo  Taasisi ya kupambana na Kuzuia Rushwa Kwa kusirikiana na Jeshi la polisi wafanye uchunguzi na ili iwapo watabainika na makosa wapelekwe mahakamani kufunguliwa mashitaka.
kuhusu bodi ya ushirika wa wakulima wa tumbaku mishamo amesema kwa mazingira hayo amezungumza na mkuu wa mkoa huo Meja Jeneral Mstaafu Raphael Muhuga kuivunja bodi ya ushirika wa wakulima wa tumbaku Mishamo  kisha iundwe bodi mpya ndani ya wiki moja itakayoweza kuwahudumia  wakulima wote.na wale wakulima waliokuwa wamefukuzwa katika ushirika huo warejeshwe na kuendelea na shughuli zao  kilimo.
Kwa upande wao Sief Elias Mbazimtima, Sesilia Emanuel , Mbonele, Emanuel Gabriel Wakabanga, wanachama wa chama cha wakulima wa tumbaku na wananchama wa TAMCOS kwa nyakati tofauti  wameeleza kukubaliana na maamuzi yaliyotolewa na mkuu wa wilaya kuhusu kuvunjwa bodi na kukamtwa wa viongozi wa TAMCOS kuwa  ni uamuzi wa busara sana.
Mwingine akaenda mbali Zaidi wamenyonywa muda mrefu lakini sasa kilio chao kimefikia mwisho kwa kuwa wamekuwa wakilima “Tunashukuru sana kwa kuwa tumekuwa tukinyonywa kwa muda mrefu kila tukilima hatupati   fadia na hatukupata mahali pa kukimbilia lakini serikali ya awamu ya tano imeweza kuwasaidia kilio chetu  alisema Mmoja wa wakulima hao”.Emanuel Gabriel Kabanga.
Awali katika Mkutano huo wa hadhara Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mpanda  Hamed Mapengo aliomba wawe watulivu pia akawataka wawe wasikivu kuusiana na majibu yaliyotolewa akawataka wakulima hao wa zao la tumbaku kutatua kero zao ambazo amezipata na kuzifanyia kazi .
Na asilimia kubwa ya wakazi wa wilaya yam panda wanatengemea zao la tumbaku laikini wakulima wamekubwa na changamoto kubwa ya umasikini pamoja na kuwa wanalima tumbaku ambalo ni zao linalotegemewa na halimashauri kuwaingia fedha na hata halmashauri inategemea sana mapato kutoka zao la tumbaku kama ushuru amBAPO Halmashauri ya Mpanda inapata mapato makubwa kutokana na zao la tumbaku.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa