Home » » WATU WAWILI JELA KIFUNGO CHA JUMLA YA MIAKA 40 JELA KWA KOSA LA MENO YA TEMBO WAANGUA KILIO KIZIMBANI BAADA YA KUHUKUMIWA

WATU WAWILI JELA KIFUNGO CHA JUMLA YA MIAKA 40 JELA KWA KOSA LA MENO YA TEMBO WAANGUA KILIO KIZIMBANI BAADA YA KUHUKUMIWA



  Na   Walter  Mguluchuma .
         Katavi .
  Mahakama  ya  Wilaya  ya   Mpanda   Mkoa  wa  Katavi  imewaukumu watu  wawili   Godfrey   Mabuga na   Rashid  Ramadhani   wakazi wa  Mtaa wa   Nsemlwa   Mjini  hapa  kutumikia   kifungo  cha jumla  ya  miaka   40  jela  baada  ya  kupatikana  na  hatia  ya  kukamatwa  na  Meno ya  Tembo  yenye  thamani  ya shilingi  milioni   48.
  Hukumu  hiyo   ilitolewa  juzi   na    Hakimu   Mkazi  mfawidhi wa  Mahakama  ya  Wilaya  ya  Mpanda   Chiganga  Ntengwa   baada  ya Mahakama   kuridhika  na  ushahidi  uluotolewa  na  upande wa  mashitaka  kwenye  kesi  hiyo.
Awali  katika   kesi  hiyo  mwendesha  mashitaka  mwanasheria  wa  Serikali  wa  Mkoa  wa  Katavi  Jamira  Mziray  alidai  washitakiwa  hao  kwa  pamoja  walitenda  kosa  hilo  hapo   Mei  20 mwaka  2014  huko  katika  eneo la  mtaa  wa  Fisi  Kata ya  Majengo  Manispaa  ya  Mpanda
Mziray  alidai kuwa  watuhimiwa  hao   siku  hiyo ya  tukio  walikamatwa  na  vipande vinne  vya   meno ya   Tembo  vyenye   thamani  ya  shilingi  milioni   48  ambapo     meno  hayo ni  sawa  na  Tembo  wawili.
 Katika  utetezi  wake   mshitakiwa   Godfrey  Mabuga   aliiomba  Mahakama   imwachie  huru kwa  kile   achodai kuwa  hakutenda  kosa  hilo  bali   alisingiziwa   tuu  na  askari  waliomkamata wa  TANAPA  na  Polisi .
Mshitakiwa   Rashid Ramadhani  katika  utetezli  wake  alidai  kuwa  siku  hiyo ya  tukio   yeye  hakuwa  mjini   Mpanda  siku  hiyo    bali    alikuwa   Usevya   Tarafa  ya  Mpimbwe   Wilayani  Mlele  hata  hivyo   alipotakiwa  kuonyesha  Tiketi ya   Basi  aliyosafiria   alishindwa   kuionyesha   Mahakamani  hapo  kama  sehemu  ya  ushahidi  wake .
Kabla  ya  kusoma   hukumu  hiyo    Hakimu  Mkazi   Chiganga  Ntengwa  aliiambia   Mahakama  kutokana  na   ushahidi  uliotolewa   Mahakamani  hapo   washitakiwa    Godfrey   Mabuga  ambae alikuwa  ndio  mshitakiwa    wa  kwanza  na   Rashid  Ramadhani   ambae  alikuwa  ni  mshitakiwa  watatu  Mahakama  imewatia  hatiani  baada ya  kupatikana  na  kosa  la kifungu   cha  sheria   Namba  86  kidogo  cha kwanza  na  cha  pili  ya uhifadhi  wa  wanyama pori   Namba  5 ya  mwaka  2009 na kfungu cha  sheria  No57 kidogo cha kwanza   sheria ya uhujumu  uchumi   sura  ya  200   marejeo ya mwaka 2000.
 Alieleza  hata  hivyo  Mahakama  hiyo   imemwachia  huru   mshitakiwa    wa  pili  baada ya  kutokuwepo   ushahidi wa kumtia   hatiani  kitendo   cha   Hakimu  kutamka  kumwachia  huru  mshitakiwa  watatu  washitakiwa  hao  waliangua  kilio  Mahakamani  hapo  huku  mshitakiwa  wa  pili  aliachiwa    akipiga  ishara ya  msalaba .


Kisha   Hakimu  Chiganga  Ntengwa    alitowa  nafasi   kwa  washitakiwa   kama   wanayosababu  yoyote ya  msingi   ya  kuishawishi   Mahakama  iliiwapunguzie  adhabu    hata   hivyo  washitakiwa  hao  walidai kuwa   hata  wakisema  wajitetea  wanajua   adhabu yao  haita  pungua  kikubwa  wanachoomba ni  kupatiwa  nakala  ya    hukumu yao .
Baada  ya  hapo  mwanasheria  wa  Serikali wa  Mkoa  wa  Katavi   Jamira   Mziray   aliiomba  Mahakama   itowe   adhabu  kali  kwa  washitakiwa  kwani kitendo cha kuuwa  Tembo  kinasababisha  wanyama  kupungua  na  kupunguza   utalii  katika   Nchi .
Hakimu   Chiganga   baada  ya  kusikiliza  pande  mbili  hizo  alisoma   hukumu  kwa  kuiambia  Mahakama   kuwa  washitakiwa  hao   wote  wawili  Mahakama  imewahukumu kila  mmoja  kutumikia  kifungo  cha  miaka   20  jela  kuanzia  juzi .

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Katavi yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa