Na Walter Mguluchuma .
Katavi yetu blog
Bodi ya shule ya Sekondari ya Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi imewafukuza shule wanafunzi 15 wa Kidato cha Sita wanaodaiwa kuwapiga walimu wao wawili kwa kuwachalaza viboko na kuwashambulia kwa silaha za jadi huku mkuu wao wa shule msaidizi kujeruhiwa vibaya kwenye sehemu zake za mwili na kung-olewa meno yake matano ya mbele .
Kikao cha Bodi hiyo kilifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita ikiwa ni siku mbili baada ya gazeti hilo kuandika habari ya tukio la wanafunzi hao kuwashambulia kwa silaha za jadi zikiwemo mawe rungu na fimbo walimu hao wawili .
Tukio la wanafunzi hao wa Sekondari ya Usevya kuwapiga walimu wao lilitokea hapo Agosti 12 mwaka huu ambapo walimu wawili walijeruhiwa vibaya akiwemo Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule hiyo Makonda Ng-oka ambae aling-olewa meno yake matano na jujeruhiwa vibaya kichwani na mkononi .
Inadaiwa chanzo cha tukio hilo ni wanafunzi wa shule hiyo wa kidato cha sita shuleni hapo kutomtaka Mwalimu Ng-oka kuendelea kufundisha kwa madai ana tabia ya kuwadhalilisha wanafunzi wa kiume .
Ilielzwa kuwa katika mkasa huo wa kupigwa kwa walimu hao siku hiyo ya tukio Mwalimu huyo alikuwa nyumbani kwake na familia yake pamoja na mgeni aliyemtembelea ambae ni Mwalimu mwenzake aitwaye Gabriel Kambona .
Ghafla waliingia Wanafunzi kundi la Wanafunzi wakiwa na silaha za jadi kama fimbo ,marungu na matofali na kuishambulia familia hiyo muda huo Mwalimu Ng-aka alikuwa bafuni anaoga alisikia mayowe ya familia yake wakiomba msaada alipotoka aliwakuta ni wanafunzi wake wanawashambulia kwa silaha za jadi walipomwona walimgeukia na kuanza kumpiga hadi kupoteza fahamu .
Katika kikao hicho cha bodi kilichokaa mwishoni mwa wiki iliyopita bodi hiyo imetowa adhabu adhabu ya kuwafukuza shuleni hapo Wanafunzi hao 15 wa kidato cha sita kwa kipindi cha wiki mbili wasionekane kwenye eneo hilo.
Pia wanafunzi hao kila mmoja amepewa adhabu ya kulipa faini yashilingi elfu ishirini kila mmoja na wanatakiwa waziwasilishe pindi wanapokuwa kuwa wamemaliza adhabu yao ya kutofika shuleni hapo .
Afisa Elimu wa Mkoa wa Katavi Enersti Hinju amekili kufanyika kwa kikao cha bodi ya shule hiyo hapo Septemba 16 na taarifa za uamuzi wa kikao cha bodi hiyo tayari zipo osifini kwake .
Alisema taarifa rasmi za maamuzi ya kikao hicho cha bodi ya shule ataitowa hivi karibuni maana alikuwa nje ya Mkoa kikazi ameripoti jana Ofisini kwake .
Nae Mwalimu Gabriel Kambana ambae ni miongoni mwa Walimu walipigwa na kutolewa ngwee kichwani alisema yeye binafsi aridhiki ana adhabu hiyo waliopewa wanafunzi hao kwani ni ndogo hailingani na kosa walilo fanya .
Alisema leo hii wanafunzi wanawapiga walimu wanapewa adhabu ndogo kama hiyo jee siku mwanafunzi atakapomgomea mwalimu atapewa adhabu gani alihoji mwalimu Kambona .
Alieleza wao kama Walimu wa shule hiyo baada ya wiki moja baada ya kutokea kwa tukio hilo walikaa kikao na kupendekeza kuwa wanafunzi 15 ambao walikuwa ndio viongozi wa vurugu hizo za kuwashambulia Walimu wafukuzwe shule moja kwa moja na wanafunzi wengine zaidi ya 200 wanarudishwe makwao na lilikundi la tatu na wanafunzi ambao hawakuwa kwenye eneo la shule ndio wabaki shule waendelee na masomo .
Kambona alisema mapendekezo hayo yalipingwa na uongozi wa Halmashauri yao ya Mpimbwe pamoja na uongozi wa Wilaya ya Mlele kwa kile walichodai hawana mamlaka hayo wakati wao walimu wanayomamlaka ya kumsimamisha mwanafunzi masomo kwa kipindi cha siku 21.
0 comments:
Post a Comment