Walter Mguluchuma , Katavi
MAHAKAMA ya Wilaya ya Mlele mkoani Katavi imewahukumu watu watatu
kutumikia kifungo cha miaka 90 jela baada kupatikana na hatia ya
unyang’anyi wa kutumia silaha na kupora zaidi ya Sh milioni 6 –
Washtakiwa hao ni pamoja na Shaban Hamis (35) mkazi wa kijiji cha
Ilunde wilayani Mlele , Masoud Ramadhani (33) mkazi wa kijiji cha
Inyonga wilayani Mlele na Ramadhani Agustino (22) mkazi wa kijiji
cha Kitunda mkoani Tabora , ambapo kila mmoja atatumikia miaka 30
jela .
“Nimetoa adhabu kali kwa washtakiwa ili iwe fundisho si kwako
tu pia kwa wengine wenye tabia kama hiyo …. Kosa la unyang’anyi kwa
kutumia silaha adhabu yake ni kifungo cha miaka 30 jela kwa kila
mshtakiwa “ alisema Swai .
Mwendesha Mashtka Mkaguzi wa Polisi , Baraka Hongoli alidai kuwa
washtakiwa hao kwa pamoja walitenda kosa hilo Agosti 21 mwaka huu
saa nane usiku katika Mtaa wa Uzenga mjini Inyonga , wilayani
Mlele .
Ilidaiwa kuwa usiku huo wa tukio washtakiwa hao wakiwa na silaha
nzito aina ya AK 47 walivamia duka la mfanyabiashara , Jonas Davis
katika Mtaa wa Uzenga na kumpora zaidi ya Sh milioni 6.0-
Mwendesha Mashtaka aliongeza kuwa washtakiwa hao walikamatwa
Septemba 16 , mwaka huu wakiwa katika nyumba ya wageni Mtaa wa
Isengo mjini Inyonga, wilayani Mlele wakijiandaa kuwapora fedha
wakulima wa tumbaku .
Ilidaiwa kuwa baada ya kukamatwa na kuhojiwa walikiri kwa
maandishi kuwa walihusika na uporaji wa sh milioni 6.0- na
wakaongoza askari polisi hadi kijijini Ilunde na kuonesha
walikoificha silaha nzito aina ya AK 47.
Washtakiwa hao watatu wanakabiliwa na mashtak mwengine ambapo
wanashtakiwa kwa kosa la kuvamia nyumba ya mkazi wa kijiji cha
Kalonvya wilayani Mlele , Patrick Nchimbi na kumpora fedha taslimu
, vitu vya thamani zikiwemo vocha za muda wa hewani , vitenge na
simu za mkononi kwa pamoj vikiwa na thamani ya Sh milioni 3.1 .
Pia wanashtakiwa kwa kumjeruhi kwa kumpiga risasi mkononi mke wa
mfanyabiashara Nchimbi ambapo mshtakiwa Shaban Hamis akikabiliwa
na kesi nyingine ya kukutwa na bunduki iliyotengenezwa kienyeji
‘gobole’ na mtutu wa bunduki. .
Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo , Swai amehahirisha keso zote
mbili hilo hadi Oktoba 12 mwaka huu zitakapotajwa tena
mahakamani hapo baada ya washtakiwa hao kukana mashtaka yao .
Mwisho.
MAHAKAMA ya Wilaya ya Mlele mkoani Katavi imewahukumu watu watatu
kutumikia kifungo cha miaka 90 jela baada kupatikana na hatia ya
unyang’anyi wa kutumia silaha na kupora zaidi ya Sh milioni 6 –
Washtakiwa hao ni pamoja na Shaban Hamis (35) mkazi wa kijiji cha
Ilunde wilayani Mlele , Masoud Ramadhani (33) mkazi wa kijiji cha
Inyonga wilayani Mlele na Ramadhani Agustino (22) mkazi wa kijiji
cha Kitunda mkoani Tabora , ambapo kila mmoja atatumikia miaka 30
jela .
“Nimetoa adhabu kali kwa washtakiwa ili iwe fundisho si kwako
tu pia kwa wengine wenye tabia kama hiyo …. Kosa la unyang’anyi kwa
kutumia silaha adhabu yake ni kifungo cha miaka 30 jela kwa kila
mshtakiwa “ alisema Swai .
Mwendesha Mashtka Mkaguzi wa Polisi , Baraka Hongoli alidai kuwa
washtakiwa hao kwa pamoja walitenda kosa hilo Agosti 21 mwaka huu
saa nane usiku katika Mtaa wa Uzenga mjini Inyonga , wilayani
Mlele .
Ilidaiwa kuwa usiku huo wa tukio washtakiwa hao wakiwa na silaha
nzito aina ya AK 47 walivamia duka la mfanyabiashara , Jonas Davis
katika Mtaa wa Uzenga na kumpora zaidi ya Sh milioni 6.0-
Mwendesha Mashtaka aliongeza kuwa washtakiwa hao walikamatwa
Septemba 16 , mwaka huu wakiwa katika nyumba ya wageni Mtaa wa
Isengo mjini Inyonga, wilayani Mlele wakijiandaa kuwapora fedha
wakulima wa tumbaku .
Ilidaiwa kuwa baada ya kukamatwa na kuhojiwa walikiri kwa
maandishi kuwa walihusika na uporaji wa sh milioni 6.0- na
wakaongoza askari polisi hadi kijijini Ilunde na kuonesha
walikoificha silaha nzito aina ya AK 47.
Washtakiwa hao watatu wanakabiliwa na mashtak mwengine ambapo
wanashtakiwa kwa kosa la kuvamia nyumba ya mkazi wa kijiji cha
Kalonvya wilayani Mlele , Patrick Nchimbi na kumpora fedha taslimu
, vitu vya thamani zikiwemo vocha za muda wa hewani , vitenge na
simu za mkononi kwa pamoj vikiwa na thamani ya Sh milioni 3.1 .
Pia wanashtakiwa kwa kumjeruhi kwa kumpiga risasi mkononi mke wa
mfanyabiashara Nchimbi ambapo mshtakiwa Shaban Hamis akikabiliwa
na kesi nyingine ya kukutwa na bunduki iliyotengenezwa kienyeji
‘gobole’ na mtutu wa bunduki. .
Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo , Swai amehahirisha keso zote
mbili hilo hadi Oktoba 12 mwaka huu zitakapotajwa tena
mahakamani hapo baada ya washtakiwa hao kukana mashtaka yao .
Mwisho.
0 comments:
Post a Comment